< Joshua 3 >

1 Then Joshua got up early in the morning, and, moving on from Shittim, he and all the children of Israel came to Jordan and were there for the night before going over.
Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
2 And at the end of three days, the men in authority over the people went through the tents,
Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
3 Giving the people their orders, and saying, When you see the ark of the agreement of the Lord your God lifted up by the priests, the Levites, then get up from your places and go after it;
wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
4 But let there be a space between you and it of about two thousand cubits: come no nearer to it, so that you may see the way you have to go, for you have not been over this way before.
Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
5 And Joshua said to the people, Make yourselves holy, for tomorrow the Lord will do works of wonder among you.
Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
6 Then Joshua said to the priests, Take up the ark of the agreement and go over in front of the people. So they took up the ark of the agreement and went in front of the people.
Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
7 And the Lord said to Joshua, From now on I will give you glory in the eyes of all Israel, so that they may see that, as I was with Moses, so I will be with you.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
8 And you are to give orders to the priests who take up the ark of the agreement, and say, When you come to the edge of the waters of Jordan, go no further.
Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
9 And Joshua said to the children of Israel, Come to me here: and give ear to the words of the Lord your God.
Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
10 And Joshua said, By this you will see that the living God is among you, and that he will certainly send out from before you the Canaanite and the Hittite and the Hivite and the Perizzite and the Girgashite and the Amorite and the Jebusite.
Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
11 See, the ark of the agreement of the Lord of all the earth is going over before you into Jordan.
Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
12 So take twelve men out of the tribes of Israel, a man from every tribe.
Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
13 And when the feet of the priests who take up the ark of the Lord, the Lord of all the earth, come to rest in the waters of Jordan, the waters of Jordan will be cut off, all the waters flowing down from higher up, and will come together in a mass.
Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
14 So when the people went out from their tents to go over Jordan, the priests who took up the ark of the agreement were in front of the people;
Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
15 And when those who took up the ark came to Jordan, and the feet of the priests who took up the ark were touching the edge of the water (for the waters of Jordan are overflowing all through the time of the grain-cutting),
Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
16 Then the waters flowing down from higher up were stopped and came together in a mass a long way back at Adam, a town near Zarethan; and the waters flowing down to the sea of the Arabah, the Salt Sea, were cut off: and the people went across opposite Jericho.
maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
17 And the priests who took up the ark of the agreement of the Lord kept their places, with their feet on dry land in the middle of Jordan, while all Israel went over on dry land, till all the nation had gone over Jordan.
Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.

< Joshua 3 >