< Jonah 2 >
1 Then Jonah made prayer to the Lord his God from the inside of the fish, and said,
Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2 In my trouble I was crying to the Lord, and he gave me an answer; out of the deepest underworld I sent up a cry, and you gave ear to my voice. (Sheol )
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol )
3 For you have put me down into the deep, into the heart of the sea; and the river was round about me; all your waves and your rolling waters went over me.
Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
4 And I said, I have been sent away from before your eyes; how may I ever again see your holy Temple?
Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 The waters were circling round me, even to the neck; the deep was about me; the sea-grass was twisted round my head.
Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
6 I went down to the bases of the mountains; as for the earth, her walls were about me for ever: but you have taken up my life from the underworld, O Lord my God.
Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
7 When my soul in me was overcome, I kept the memory of the Lord: and my prayer came in to you, into your holy Temple.
“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
8 The worshippers of false gods have given up their only hope.
“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 But I will make an offering to you with the voice of praise; I will give effect to my oaths. Salvation is the Lord's.
Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
10 And at the Lord's order, the fish sent Jonah out of its mouth on to the dry land.
Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.