< Job 28 >

1 Truly there is a mine for silver, and a place where gold is washed out.
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
2 Iron is taken out of the earth, and stone is changed into brass by the fire.
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
3 Man puts an end to the dark, searching out to the farthest limit the stones of the deep places of the dark.
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
4 He makes a deep mine far away from those living in the light of day; when they go about on the earth, they have no knowledge of those who are under them, who are hanging far from men, twisting from side to side on a cord.
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
5 As for the earth, bread comes out of it; but under its face it is turned up as if by fire.
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
6 Its stones are the place of sapphires, and it has dust of gold.
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
7 No bird has knowledge of it, and the hawk's eye has never seen it.
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
8 The great beasts have not gone over it, and the cruel lion has not taken that way.
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
9 Man puts out his hand on the hard rock, overturning mountains by the roots.
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
10 He makes deep ways, cut through the rock, and his eye sees everything of value.
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
11 He keeps back the streams from flowing, and makes the secret things come out into the light.
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
12 But where may wisdom be seen? and where is the resting-place of knowledge?
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
13 Man has not seen the way to it, and it is not in the land of the living.
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
14 The deep waters say, It is not in me: and the sea says, It is not with me.
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
15 Gold may not be given for it, or a weight of silver in payment for it.
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
16 It may not be valued with the gold of Ophir, with the onyx of great price, or the sapphire.
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
17 Gold and glass are not equal to it in price, and it may not be exchanged for jewels of the best gold.
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
18 There is no need to say anything about coral or crystal; and the value of wisdom is greater than that of pearls.
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
19 The topaz of Ethiopia is not equal to it, and it may not be valued with the best gold.
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
20 From where then does wisdom come, and where is the resting-place of knowledge?
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
21 For it is kept secret from the eyes of all living, unseen by the birds of the air.
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
22 Destruction and Death say, We have only had word of it with our ears.
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
23 God has knowledge of the way to it, and of its resting-place;
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
24 For his eyes go to the ends of the earth, and he sees everything under heaven.
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
25 When he made a weight for the wind, measuring out the waters;
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
26 When he made a law for the rain, and a way for the thunder-flames;
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
27 Then he saw it, and put it on record; he gave it its fixed form, searching it out completely.
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
28 And he said to man, Truly the fear of the Lord is wisdom, and to keep from evil is the way to knowledge.
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”

< Job 28 >