< Jeremiah 8 >
1 At that time, says the Lord, they will take the bones of the kings of Judah, and the bones of his rulers, and the bones of the priests, and the bones of the prophets, and the bones of the people of Jerusalem out of their resting-places:
“‘Wakati huo, asema Bwana, mifupa ya wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, na mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka makaburi yao.
2 And they will put them out before the sun and the moon and all the stars of heaven, whose lovers and servants they have been, after whom they have gone, to whom they have made prayers, and to whom they have given worship: they will not be put together or placed in the earth; they will be waste on the face of the earth.
Itawekwa wazi kwa jua, na mwezi, na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia, na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyotapakaa juu ya ardhi.
3 And death will be desired more than life by the rest of this evil family who are still living in all the places where I have sent them away, says the Lord of armies.
Popote nitakapowafukuzia, mabaki wote wa kizazi hiki kiovu watatamani kufa kuliko kuishi, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
4 Further, you are to say to them, This is what the Lord has said: Will those who are falling not be lifted up again? will he who has gone away not come back?
“Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “‘Je, watu wanapoanguka hawainuki? Je, mtu anapopotea harudi?
5 Why do these people of Jerusalem go back, for ever turning away? they will not give up their deceit, they will not come back.
Kwa nini basi watu hawa walipotea? Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara? Wanangʼangʼania udanganyifu na wanakataa kurudi.
6 I took note and gave ear, but no one said what is right: no man had regret for his evil-doing, saying, What have I done? everyone goes off on his way like a horse rushing to the fight.
Nimewasikiliza kwa makini, lakini hawataki kusema lililo sawa. Hakuna anayetubia makosa yake akisema, “Nimefanya nini?” Kila mmoja hufuata njia yake mwenyewe kama farasi anayekwenda vitani.
7 Truly, the stork in the heavens is conscious of her fixed times; the dove and the swallow and the crane keep to the times of their coming; but my people have no knowledge of the law of the Lord.
Hata korongo aliyeko angani anayajua majira yake yaliyoamriwa, nao njiwa, mbayuwayu na koikoi hufuata majira yao ya kurudi. Lakini watu wangu hawajui Bwana anachotaka kwao.
8 How is it that you say, We are wise and the law of the Lord is with us? But see, the false pen of the scribes has made it false.
“‘Mwawezaje kusema, “Sisi tuna busara kwa sababu tunayo sheria ya Bwana,” wakati ambapo kwa hakika kalamu ya uongo ya waandishi imeandika kwa udanganyifu?
9 The wise men are shamed, they are overcome with fear and taken: see, they have given up the word of the Lord; and what use is their wisdom to them?
Wenye hekima wataaibika, watafadhaika na kunaswa. Kwa kuwa wamelikataa neno la Bwana, hiyo hekima waliyo nayo ni ya namna gani?
10 So I will give their wives to others, and their fields to those who will take them for themselves: for everyone, from the least to the greatest, is given up to getting money; from the priest even to the prophet, everyone is false.
Kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao, na mashamba yao kwa wamiliki wengine. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
11 And they have made little of the wounds of the daughter of Zion, saying, Peace, peace; when there is no peace.
Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, “Amani, amani,” wakati hakuna amani.
12 Let them be put to shame because they have done disgusting things. They had no shame, they were not able to become red with shame: so they will come down with those who are falling: in the time of their punishment they will be made low, says the Lord.
Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo, hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini watakapoadhibiwa, asema Bwana.
13 I will put an end to them completely, says the Lord: there are no grapes on the vine and no figs on the fig-tree, and the leaf is dry.
“‘Nitayaondoa mavuno yao, asema Bwana. Hapatakuwepo zabibu kwenye mzabibu. Hapatakuwepo na tini kwenye mtini, majani yake yatanyauka. Kile nilichowapa watanyangʼanywa.’”
14 Why are we seated doing nothing? come together, and let us go to the walled towns, and let destruction overtake us there, for the Lord our God has sent destruction on us, and given us bitter water for our drink, because we have done evil against the Lord.
“Kwa nini tunaketi hapa? Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie kwenye miji yenye maboma, tukaangamie huko! Kwa kuwa Bwana, Mungu wetu ametuhukumu kuangamia, na kutupa maji yenye sumu tunywe, kwa sababu tumemtenda dhambi.
15 We were looking for peace, but no good came; and for a time of well-being, but there is only a great fear.
Tulitegemea amani, lakini hakuna jema lililokuja, tulitegemea wakati wa kupona, lakini kulikuwa hofu tu.
16 The loud breathing of the horses comes to our ears from Dan: at the sound of the outcry of his war-horses, all the land is shaking with fear; for they have come, and have made a meal of the land and everything in it; the town and the people living in it.
Mkoromo wa farasi za adui umesikika kuanzia Dani, kwa mlio wa madume yao ya farasi, nchi yote inatetemeka. Wamekuja kuangamiza nchi na vyote vilivyomo, mji na wote waishio ndani yake.”
17 See, I will send snakes and poison-snakes among you, against which the wonder-worker has no power; and they will give you wounds which may not be made well, says the Lord.
“Tazama, nitatuma nyoka wenye sumu kali katikati yenu, fira ambao hawawezi kulogwa, nao watawauma,” asema Bwana.
18 Sorrow has come on me! my heart in me is feeble.
Ee Mfariji wangu katika huzuni, moyo wangu umezimia ndani yangu.
19 The voice of the cry of the daughter of my people comes from a far land: Is the Lord not in Zion? is not her King in her? Why have they made me angry with their images and their strange gods which are no gods?
Sikia kilio cha watu wangu kutoka nchi ya mbali: “Je, Bwana hayuko Sayuni? Je, Mfalme wake hayuko tena huko?” “Kwa nini wamenikasirisha kwa vinyago vyao, kwa sanamu zao za kigeni zisizofaa?”
20 The grain-cutting is past, the summer is ended, and no salvation has come to us.
“Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha, nasi hatujaokolewa.”
21 For the destruction of the daughter of my people I am broken: I am dressed in the clothing of grief; fear has taken me in its grip.
Kwa kuwa watu wangu wamepondwa, nami nimepondeka pia; ninaomboleza, nayo hofu kuu imenishika.
22 Is there no life-giving oil in Gilead? is there no expert in medical arts? why then have my people not been made well?
Je, hakuna zeri ya kuponya katika Gileadi? Je, hakuna tabibu huko? Kwa nini basi hakuna uponyaji wa majeraha ya watu wangu?