< Jeremiah 44 >

1 The word which came to Jeremiah about all the Jews who were living in the land of Egypt, in Migdol and at Tahpanhes and at Noph and in the country of Pathros, saying,
Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
2 The Lord of armies, the God of Israel, has said: You have seen all the evil which I have sent on Jerusalem and on all the towns of Judah; and now, this day they are waste and unpeopled;
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
3 Because of the evil which they have done, moving me to wrath by burning perfumes in worship to other gods, who were not their gods or yours or the gods of their fathers.
kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
4 And I sent all my servants the prophets to you, getting up early and sending them, saying, Do not do this disgusting thing which is hated by me.
Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
5 But they gave no attention, and their ears were not open so that they might be turned from their evil-doing and from burning perfume to other gods.
Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
6 Because of this, my passion and my wrath were let loose, burning in the towns of Judah and in the streets of Jerusalem; and they are waste and unpeopled as at this day.
Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
7 So now, the Lord, the God of armies, the God of Israel, has said, Why are you doing this great evil against yourselves, causing every man and woman, little child and baby at the breast among you in Judah to be cut off till not one is still living;
“Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
8 Moving me to wrath with the work of your hands, burning perfumes to other gods in the land of Egypt, where you have gone to make a place for yourselves, so that you may become a curse and a name of shame among all the nations of the earth?
Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
9 Have you no memory of the evil-doing of your fathers, and the evil-doing of the kings of Judah, and the evil-doing of their wives, and the evil which you yourselves have done, and the evil which your wives have done, in the land of Judah and in the streets of Jerusalem?
Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
10 Even to this day their hearts are not broken, and they have no fear, and have not gone in the way of my law or of my rules which I gave to you and to your fathers.
Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
11 So this is what the Lord of armies, the God of Israel, has said: See, my face will be turned against you for evil, for the cutting off of all Judah;
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
12 And I will take the last of Judah, whose minds are fixed on going into the land of Egypt and stopping there, and they will all come to their end, falling in the land of Egypt by the sword and by being short of food and by disease; death will overtake them, from the least to the greatest, death by the sword and by need of food: they will become an oath and a cause of wonder and a curse and a name of shame.
Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
13 For I will send punishment on those who are living in the land of Egypt, as I have sent punishment on Jerusalem, by the sword and by need of food and by disease:
Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
14 So that not one of the rest of Judah, who have gone into the land of Egypt and are living there, will get away or keep his life, to come back to the land of Judah where they are hoping to come back and be living again: for not one will come back, but only those who are able to get away.
Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
15 Then all the men who had knowledge that their wives were burning perfumes to other gods, and all the women who were present, a great meeting, answering Jeremiah, said,
Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
16 As for the word which you have said to us in the name of the Lord, we will not give ear to you.
“Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
17 But we will certainly do every word which has gone out of our mouths, burning perfumes to the queen of heaven and draining out drink offerings to her as we did, we and our fathers and our kings and our rulers, in the towns of Judah and in the streets of Jerusalem: for then we had food enough and did well and saw no evil.
Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
18 But from the time when we gave up burning perfumes to the queen of heaven and draining out drink offerings to her, we have been in need of all things, and have been wasted by the sword and by need of food.
Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
19 And the women said, When we were burning perfumes to the queen of heaven and draining out drink offerings to her, did we make cakes in her image and give her our drink offerings without the knowledge of our husbands?
Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
20 Then Jeremiah said to all the people, to the men and women and all the people who had given him that answer,
Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
21 The perfumes which you have been burning in the towns of Judah and in the streets of Jerusalem, you and your fathers and your kings and your rulers and the people of the land, had the Lord no memory of them, and did he not keep them in mind?
“Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
22 And the Lord was no longer able to put up with the evil of your doings and the disgusting things you did; and because of this your land has become a waste and a cause of wonder and a curse, with no one living in it, as at this day.
Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
23 Because you have been burning perfumes, and sinning against the Lord, and have not given ear to the voice of the Lord, or gone in the way of his law or his rules or his orders; for this reason this evil has come on you, as it is today.
Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
24 Further, Jeremiah said to all the people and all the women, Give ear to the word of the Lord, all those of Judah who are living in Egypt:
Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
25 This is what the Lord of armies, the God of Israel, has said: You women have said with your mouths, and with your hands you have done what you said, We will certainly give effect to the oaths we have made, to have perfumes burned to the queen of heaven and drink offerings drained out to her: then give effect to your oaths and do them.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
26 And now give ear to the word of the Lord, all you of Judah who are living in the land of Egypt: Truly, I have taken an oath by my great name, says the Lord, that my name is no longer to be named in the mouth of any man of Judah in all the land of Egypt, saying, By the life of the Lord God.
Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
27 See, I am watching over them for evil and not for good: all the men of Judah who are in the land of Egypt will be wasted by the sword and by need of food till there is an end of them.
Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
28 And those who get away safe from the sword will come back from the land of Egypt to the land of Judah, a very small number; and all the rest of Judah, who have gone into the land of Egypt and are living there, will see whose word has effect, mine or theirs.
Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
29 And this will be the sign to you, says the Lord, that I will give you punishment in this place, so that you may see that my words will certainly have effect against you for evil:
“‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
30 The Lord has said, See, I will give up Pharaoh Hophra, king of Egypt, into the hands of those who are fighting against him and desiring to take his life, as I gave Zedekiah, king of Judah, into the hands of Nebuchadrezzar, king of Babylon, his hater, who had designs against his life.
Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”

< Jeremiah 44 >