< Jeremiah 33 >

1 Then the word of the Lord came to Jeremiah the second time, while he was still shut up in the place of the armed watchmen, saying,
Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
2 These are the words of the Lord, who is doing it, the Lord who is forming it, to make it certain; the Lord is his name;
“Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
3 Let your cry come to me, and I will give you an answer, and let you see great things and secret things of which you had no knowledge.
‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
4 For this is what the Lord, the God of Israel, has said about the houses of this town and the houses of the kings of Judah, which have been broken down to make earthworks and ...;
Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
5 ... and to make them full of the dead bodies of men whom I have put to death in my wrath and in my passion, and because of whose evil-doing I have kept my face covered from this town.
katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
6 See, I will make it healthy and well again, I will even make them well; I will let them see peace and good faith in full measure.
“‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
7 And I will let the fate of Judah and of Israel be changed, building them up as at first.
Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
8 And I will make them clean from all their sin, with which they have been sinning against me; I will have forgiveness for all their sins, with which they have been sinning against me, and with which they have done evil against me.
Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
9 And this town will be to me for a name of joy, for a praise and a glory before all the nations of the earth, who, hearing of all the good which I am doing for them, will be shaking with fear because of all the good and the peace which I am doing for it.
Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
10 This is what the Lord has said: There will again be sounding in this place, of which you say, It is a waste, without man and without beast; even in the towns of Judah and in the streets of Jerusalem which are waste and unpeopled, without man and without beast,
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
11 Happy sounds, the voice of joy, the voice of the newly-married man and the voice of the bride, the voices of those who say, Give praise to the Lord of armies, for the Lord is good, for his mercy is unchanging for ever: the voices of those who go with praise into the house of the Lord. For I will let the land come back to its first condition, says the Lord.
sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
12 This is what the Lord of armies has said: Again there will be in this place, which is a waste, without man and without beast, and in all its towns, a resting-place where the keepers of sheep will make their flocks take rest.
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
13 In the towns of the hill-country, in the towns of the lowland, and in the towns of the South and in the land of Benjamin and in the country round Jerusalem and in the towns of Judah, the flocks will again go under the hand of him who is numbering them, says the Lord.
Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
14 See, the days are coming, says the Lord, when I will give effect to the good word which I have said about the people of Israel and the people of Judah.
“‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
15 In those days and at that time, I will let a Branch of righteousness come up for David; and he will be a judge in righteousness in the land.
“‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
16 In those days, Judah will have salvation and Jerusalem will be safe: and this is the name which will be given to her: The Lord is our righteousness.
Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
17 For the Lord has said, David will never be without a man to take his place on the seat of the kingdom of Israel;
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
18 And the priests and the Levites will never be without a man to come before me, offering burned offerings and perfumes and meal offerings and offerings of beasts at all times.
wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
19 And the word of the Lord came to Jeremiah, saying,
Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
20 The Lord has said: If it is possible for my agreement of the day and the night to be broken, so that day and night no longer come at their fixed times,
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
21 Then my agreement with my servant David may be broken, so that he no longer has a son to take his place on the seat of the kingdom; and my agreement with the Levites, the priests, my servants.
basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
22 As it is not possible for the army of heaven to be numbered, or the sand of the sea measured, so will I make the seed of my servant David, and the Levites my servants.
Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
23 And the word of the Lord came to Jeremiah, saying,
Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
24 Have you taken note of what these people have said, The two families, which the Lord took for himself, he has given up? This they say, looking down on my people as being, in their eyes, no longer a nation.
“Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
25 The Lord has said, If I have not made day and night, and if the limits of heaven and earth have not been fixed by me,
Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
26 Then I will give up caring for the seed of Jacob and of David my servant, so that I will not take of his seed to be rulers over the seed of Abraham, Isaac, and Jacob: for I will let their fate be changed and will have mercy on them.
basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”

< Jeremiah 33 >