< Isaiah 22 >

1 The word about the valley of vision. Why have all your people gone up to the house-tops?
Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
2 You, who are full of loud voices, a town of outcries, given up to joy; your dead men have not been put to the sword, or come to their death in war.
Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
3 All your rulers ... have gone in flight; all your strong ones have gone far away.
Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
4 For this cause I have said, Let your eyes be turned away from me in my bitter weeping; I will not be comforted for the wasting of the daughter of my people.
Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
5 For it is a day of trouble and of crushing down and of destruction from the Lord, the Lord of armies, in the valley of vision; ...
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
6 And Elam was armed with arrows, and Aram came on horseback; and the breastplate of Kir was uncovered.
Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
7 And your most fertile valleys were full of war-carriages, and the horsemen took up their positions in front of the town.
Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
8 He took away the cover of Judah; and in that day you were looking with care at the store of arms in the house of the woods.
ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
9 And you saw all the broken places in the wall of the town of David: and you got together the waters of the lower pool.
mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
10 And you had the houses of Jerusalem numbered, pulling down the houses to make the wall stronger.
Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
11 And you made a place between the two walls for storing the waters of the old pool: but you gave no thought to him who had done this, and were not looking to him by whom it had been purposed long before.
Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
12 And in that day the Lord, the Lord of armies, was looking for weeping, and cries of sorrow, cutting off of the hair, and putting on the clothing of grief:
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
13 But in place of these there was joy and delight, oxen and sheep were being made ready for food, there was feasting and drinking: men said, Now is the time for food and wine, for tomorrow death comes.
Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
14 And the Lord of armies said to me secretly, Truly, this sin will not be taken from you till your death, says the Lord, the Lord of armies.
Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
15 The Lord, the Lord of armies, says, Go to this person in authority, this Shebna, who is over the house; who has made himself a resting-place on high, cutting out a place for himself in the rock, and say,
Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
16 Who are you, and by what right have you made for yourself a resting-place here?
Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
17 See, O strong man, the Lord will send you violently away, gripping you with force,
“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
18 Twisting you round and round like a ball he will send you out into a wide country: there you will come to your end, and there will be the carriages of your pride, O shame of your lord's house!
Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
19 And I will have you forced out of your place of authority, and pulled down from your position.
Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
20 And in that day I will send for my servant, Eliakim, the son of Hilkiah:
“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
21 And I will put your robe on him, and put your band about him, and I will give your authority into his hand: and he will be a father to the men of Jerusalem, and to the family of Judah.
Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
22 And I will give the key of the family of David into his care; and what he keeps open will be shut by no one, and what he keeps shut no one will make open.
Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
23 And I will put him like a nail in a safe place; and he will be for a seat of glory to his father's family.
Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
24 And all the glory of his father's family will be hanging on him, all their offspring, every small vessel, even the cups and the basins.
Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
25 In that day, says the Lord of armies, will the nail fixed in a safe place give way; and it will be cut down, and in its fall the weight hanging on it will be cut off, for the Lord has said it.
Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.

< Isaiah 22 >