< Genesis 48 >

1 Now after these things, word came to Joseph that his father was ill: and he took with him his sons Manasseh and Ephraim.
Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
2 And when they said to Jacob, Your son Joseph is coming to see you: then Israel, getting all his strength together, had himself lifted up in his bed.
Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
3 And Jacob said to Joseph, God, the Ruler of all, came to me in a vision at Luz in the land of Canaan, and gave me his blessing,
Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
4 And said to me, Truly, I will make you fertile and give you increase and will make of you a great family of nations: and I will give this land to your seed after you to be their heritage for ever.
naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
5 And now your two sons who came to birth in Egypt before I came to you here, are mine; Ephraim and Manasseh will be mine, in the same way as Reuben and Simeon are.
“Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
6 And any other offspring which you have after them, will be yours, and will be named after their brothers in their heritage.
Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
7 And as for me, when I came from Paddan, death overtook Rachel on the way, when we were still some distance from Ephrath; and I put her to rest there on the road to Ephrath, which is Beth-lehem.
Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
8 Then Israel, looking at Joseph's sons, said, Who are these?
Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
9 And Joseph said to his father, They are my sons, whom God has given me in this land. And he said, Let them come near me, and I will give them a blessing.
Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
10 Now because Israel was old, his eyes were no longer clear, and he was not able to see. So he made them come near to him, and he gave them a kiss, folding them in his arms.
Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
11 And Israel said to Joseph, I had no hope of seeing your face again, but God in his mercy has let me see you and your children.
Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
12 Then Joseph took them from between his knees, and went down on his face to the earth.
Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
13 Then taking Ephraim with his right hand, Joseph put him at Israel's left side, and with his left hand he put Manasseh at Israel's right side, placing them near him.
Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
14 And Israel, stretching out his right hand, put it on the head of Ephraim, the younger, and his left hand on the head of Manasseh, crossing his hands on purpose, for Manasseh was the older.
Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
15 And he gave Joseph a blessing, saying, May the God to whom my fathers, Abraham and Isaac, gave worship, the God who has taken care of me all my life till this day,
Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
16 The angel who has been my saviour from all evil, send his blessing on these children: and let my name and the name of my fathers, Abraham and Isaac, be given to them; and let them become a great nation in the earth.
Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
17 Now when Joseph saw that his father had put his right hand on the head of Ephraim, it did not seem right to him; and lifting his father's hand he would have put it on the head of Manasseh.
Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
18 And Joseph said to his father, Not so, my father, for this is the older; put your right hand on his head.
Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
19 But his father would not, saying, I am doing it on purpose, my son; he will certainly become a nation and a great one; but his younger brother will be greater than he, and his seed will become a great family of nations.
Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
20 So he gave them his blessing that day, saying, You will be the sign of blessing in Israel, for they will say, May God make you like Ephraim and Manasseh; and he put Ephraim before Manasseh.
Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
21 Then Israel said to Joseph, Now my death is near; but God will be with you, guiding you back to the land of your fathers.
Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
22 And I have given you more than your brothers, even Shechem as your heritage, which I took from the Amorites with my sword and my bow.
Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

< Genesis 48 >