< Ezekiel 46 >
1 This is what the Lord has said: The doorway of the inner square looking to the east is to be shut on the six working days; but on the Sabbath it is to be open, and at the time of the new moon it is to be open.
Bwana Yahwe asema hivi: Lango la uzio wa ndani, linaloelekea mashariki, litafungwa kwa mda wa siku sita za kazi, lakini katika siku za Sabato litakuwa wazi, na katika siku ya mwezi mpya litafunguliwa.
2 And the ruler is to go in through the covered way of the outer doorway outside, and take his place by the pillar of the doorway, and the priests will make his burned offering and his peace-offerings and he will give worship at the doorstep of the doorway; then he will go out, and the door will not be shut till the evening.
Mwana wa mfalme ataingia kwa kutumia lango la njia ya nyuma ya varanda upande wa nje, na atasimama mbele ya muhimili wa mwimo wa lango la ndani wakati makuhani wakiwa wakitengeza sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani. Kisha ataabudu kwenye kizingiti cha lango la ndani na kutoka nje, lakini lango halitakuwa linafungwa hadi jioni.
3 And the people of the land are to give worship at the door of that doorway before the Lord on the Sabbaths and at the new moons.
Watu wa nchi pia wataabudu mbele ya Yahwe kwenye hili lango la kuingilia katika siku ya Sabato na siku mpya za mwezi.
4 And the burned offering offered to the Lord by the ruler on the Sabbath day is to be six lambs without a mark on them and a male sheep without a mark;
Sadaka ya kuteketezwa ambayo mwana wa mfalme aitoayo kwa Yahwe katika siku ya Sabato itakuwa wanakondoo sita wasiokuwa na dosari na kondoo dume asiyekuwa na dosari.
5 And the meal offering is to be an ephah for the sheep, and for the lambs whatever he is able to give, and a hin of oil to an ephah.
Sadaka ya unga pamoja na kondoo dume itakuwa efa moja, na sadaka ya unga pamoja na wanakondoo kiasi awezacho kutoa, na hini moja ya mafuta pamoja na kila efa ya unga.
6 And at the time of the new moon it is to be a young ox of the herd without a mark on him, and six lambs and a male sheep, all without a mark:
Katika siku ya mwezi mpya atatoa ng'ombe mchanga asiyekuwa na dosari kutoka kuchungwa, wanakondoo sita, na kondoo asyekuwa na dosari.
7 And he is to give a meal offering, an ephah for the ox and an ephah for the sheep, and for the lambs whatever he is able to give, and a hin of oil to an ephah.
Atatengeneza sadaka ya unga ya efa moja kwa ajili ya ng'ombe na efa moja kwa ajili ya kondoo, na kwa kiasi awezacho kukitoa kwa ajili ya wanakondoo, na hini ya mafuta kwa kila efa ya unga.
8 And when the ruler comes in, he is to go in through the covered way of the doorway, and he is to go out by the same way.
Wakati mwana wa mfalme atakapokuwa anaingia kwa njia ya lango lenye varanda, ataondoka kwa njia hiyo hiyo.
9 But when the people of the land come before the Lord at the fixed feasts, he who comes in by the north doorway to give worship is to go out by the south doorway; and he who comes in by the south doorway is to go out by the north doorway: he is not to come back by the doorway through which he went in, but is to go straight before him.
Lakini wakati watu wa nchi watakakuja kwa Yahwe katika sikukuu zilizoteuliwa, kila mmoja kuingia kupitia kwenye lango la kaskazini kuabudu ataondoka kupitia lango la kusini; na kila atakayeingillia kupitia lango la kusini atatoka kupitia lango la kaskazini. Hakuna atakayerudia kwa lile lango aliloingilia, kwa kuwa atatoka nje moja kwa moja.
10 And the ruler, when they come in, is to come among them, and is to go out when they go out.
Mwana wa mfalme atakuwa kati yao; watakapoingia, ataingia ndani, na watakapoondoka, atatoka nao.
11 At the feasts and the fixed meetings the meal offerings are to be an ephah for an ox, and an ephah for a male sheep, and for the lambs whatever he is able to give, and a hin of oil to an ephah.
Kwenye sikukuu hizo, sadaka ya unga itakuwa efa moja ya unga kwa ng'ombe mmoja na efa moja kwa kondoo dume, na chochote atakacho kitoa pamoja na wanakondoo, na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
12 And when the ruler makes a free offering, a burned offering or a peace-offering freely given to the Lord, the doorway looking to the east is to be made open for him, and he is to make his burned offering and his peace-offerings as he does on the Sabbath day: and he will go out; and the door will be shut after he has gone out.
Wakati mwana wa mfalme atakapotoa sadaka atakayojisikia kutoa, labda sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani kwa Yahwe, lango la kuelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka ya amani kama afanyavyo siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, na baada ya kutoka lango litafungwa.
13 And you are to give a lamb a year old without any mark on it for a burned offering to the Lord every day: morning by morning you are to give it.
Kwa kuongeza, utatoa mwanakondoo asiyekuwa na dosari mwenye umri wa mwaka mmoja kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe kila siku; utafanya hivi kila asubuhi.
14 And you are to give, morning by morning, a meal offering with it, a sixth of an ephah and a third of a hin of oil dropped on the best meal; a meal offering offered to the Lord at all times by an eternal order.
Utatoa sadaka ya unga pamoja nayo kila asubuhi, efa sita na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta kuchanganya na sadaka ya unga kwa ajili ya Yahwe, kulingana na sheria ilivyo.
15 And they are to give the lamb and the meal offering and the oil, morning by morning, for a burned offering at all times.
Watandaa mwanakondoo, sadaka ya kuteketezwa, na mafuta kila asubuhi, sadaka ya kuteketezwa ya kudumu.
16 This is what the Lord has said: If the ruler gives a property to any of his sons, it is his heritage and will be the property of his sons; it is theirs for their heritage.
Bwana Yahwe asema hivi: Kama mwana wa mfalme akitoa zawadi kwa mmoja wa watoto wake, imekuwa urithi wake. Itakuwa mali ya mtoto wake, imekuwa urithi.
17 And if he gives a part of his heritage to one of his servants, it will be his till the year of making free, and then it will go back to the ruler; for it is his sons' heritage, and is to be theirs.
Lakini kama akimpatia zawadi kutoka urithi wake kwa mmoja wa watumishi wake, kisha itakuwa ya huyo mtumishi mpaka mwaka wa uhuru, na kisha itarudi kwa mwana wa mfalme. Urithi wake yamkini ukawa kwa ajili ya watoto wake.
18 And the ruler is not to take the heritage of any of the people, driving them out of their property; he is to give a heritage to his sons out of the property which is his: so that my people may not be sent away from their property.
Mwana wa mfalme hatawaondolea urithi wa watu kutoka kwenye mali zao wenyewe; ataandaa kwa ajili ya watoto wake mali ili kwamba watu wangu wasitawanyike, kila mtu kutoka mali kwenye yake mwenyewe.”
19 And he took me through by the way in at the side of the doorway into the holy rooms which are the priests', looking to the north: and I saw a place at the side of them to the west.
Kisha yule mtu akaniletea kwenye lango la kutokea hata kwenye vyumba vitakatifu kwa ajili ya makuhani, vilivyokuwa vimeelekea kaskazini na tazama! Kulikuwa na sehemu mbele magharibi.
20 And he said to me, This is the place where the offering for error and the sin-offering are to be cooked in water by the priests, and where the meal offering is to be cooked in the oven; so that they may not be taken out into the outer square to make the people holy.
Akanambia, “Hii ndio sehemu ambayo makuhani watakapo chemshia sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na walipookea sadaka ya unga. Wasilete sadaka nje ya uzio, kwa kuwa watu watatakaswa.”
21 And he took me out into the outer square and made me go by the four angles of the square; and I saw that in every angle of the open square there was a space shut in.
Kisha akanileta kwenye uzio wa nje akaniongoza kuzunguka pembe nne za uzio, nikaona kwamba katika kila pembe ya uzio kulikuwa na uwanja.
22 In the four angles there were spaces walled in, forty cubits long and thirty wide; the four were of the same size.
Katika hizo pembe nne za nje ya uzio kulikuwa na nzio nne ndogo, dhiraa arobaini urefu na thelathini upana. Ukubwa ule ule kwa nzio zote nne.
23 And there was a line of wall all round inside them, round all four, and boiling-places were made under it all round about.
Kulikuwa na safu zilizokuwa zimetengenezwa kwa mawe kuzizunguka zote nne, na meko ya kupikia ilikuwa chini ya safu ya jiwe.
24 And he said to me, These are the boiling-rooms, where the offering of the people is cooked by the servants of the house.
Yule mtu akanambia, “Hizi ndizo sehemu ambazo watumishi watachemshia dhabihu za watu.”