< Ezekiel 11 >
1 And the wind, lifting me up, took me to the east doorway of the Lord's house, looking to the east: and at the door I saw twenty-five men; and among them I saw Jaazaniah, the son of Azzur, and Pelatiah, the son of Benaiah, rulers of the people.
Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
2 Then he said to me, Son of man, these are the men who are designing evil, who are teaching evil ways in this town:
Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
3 Who say, This is not the time for building houses: this town is the cooking-pot and we are the flesh.
Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
4 For this cause be a prophet against them, be a prophet, O son of man.
Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
5 And the spirit of the Lord came on me, and he said to me, Say, These are the words of the Lord: This is what you have said, O children of Israel; what comes into your mind is clear to me.
Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
6 You have made great the number of your dead in this town, you have made its streets full of dead men.
Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
7 For this reason the Lord has said: Your dead whom you have put down in its streets, they are the flesh, and this town is the cooking-pot: but I will make you come out from inside it.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
8 You have been fearing the sword, and I will send the sword on you, says the Lord.
Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
9 I will make you come out from inside the town and will give you up into the hands of men from other lands, and will be judge among you.
Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
10 You will come to your death by the sword; and I will be your judge in the land of Israel; and you will be certain that I am the Lord.
Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
11 This town will not be your cooking-pot, and you will not be the flesh inside it; I will be your judge at the limit of the land of Israel;
Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
12 And you will be certain that I am the Lord: for you have not been guided by my rules or given effect to my orders, but you have been living by the orders of the nations round about you.
Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
13 Now while I was saying these things, death came to Pelatiah, the son of Benaiah. Then falling down on my face and crying out with a loud voice, I said, Ah, Lord! will you put an end to all the rest of Israel?
Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
14 And the word of the Lord came to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
15 Son of man, your countrymen, your relations, and all the children of Israel, all of them, are those to whom the people of Jerusalem have said, Go far from the Lord; this land is given to us for a heritage:
“Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
16 For this reason say, This is what the Lord has said: Though I have had them moved far off among the nations, and though I have sent them wandering among the countries, still I have been a safe place for them for a little time in the countries where they have come.
“Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
17 Then say, This is what the Lord has said: I will get you together from the peoples, and make you come out of the countries where you have been sent in flight, and I will give you the land of Israel.
“Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
18 And they will come there, and take away all the hated and disgusting things from it.
“Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
19 And I will give them a new heart, and I will put a new spirit in them; and I will take the heart of stone out of their flesh and give them a heart of flesh:
Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
20 So that they may be guided by my rules and keep my orders and do them: and they will be to me a people, and I will be to them a God.
Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
21 But as for those whose heart goes after their hated and disgusting things, I will send on their heads the punishment of their ways, says the Lord.
Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
22 Then the wings of the winged ones were lifted up, and the wheels were by their side; and the glory of the God of Israel was over them on high.
Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
23 And the glory of the Lord went up from inside the town, and came to rest on the mountain on the east side of the town.
Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
24 And the wind, lifting me up, took me in the visions of God into Chaldaea, to those who had been taken away as prisoners. So the vision which I had seen went away from me.
Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
25 Then I gave an account to those who had been taken prisoners of all the things which the Lord had made me see.
nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.