< Exodus 12 >
1 And the Lord said to Moses and Aaron in the land of Egypt,
Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
2 Let this month be to you the first of months, the first month of the year.
“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
3 Say to all the children of Israel when they are come together, In the tenth day of this month every man is to take a lamb, by the number of their fathers' families, a lamb for every family:
Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
4 And if the lamb is more than enough for the family, let that family and its nearest neighbour have a lamb between them, taking into account the number of persons and how much food is needed for every man.
Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
5 Let your lamb be without a mark, a male in its first year: you may take it from among the sheep or the goats:
Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
6 Keep it till the fourteenth day of the same month, when everyone who is of the children of Israel is to put it to death between sundown and dark.
Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
7 Then take some of the blood and put it on the two sides of the door and over the door of the house where the meal is to be taken.
Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
8 And let your food that night be the flesh of the lamb, cooked with fire in the oven, together with unleavened bread and bitter-tasting plants.
Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
9 Do not take it uncooked or cooked with boiling water, but let it be cooked in the oven; its head with its legs and its inside parts.
Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
10 Do not keep any of it till the morning; anything which is not used is to be burned with fire.
Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
11 And take your meal dressed as if for a journey, with your shoes on your feet and your sticks in your hands: take it quickly: it is the Lord's Passover.
Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
12 For on that night I will go through the land of Egypt, sending death on every first male child, of man and of beast, and judging all the gods of Egypt: I am the Lord.
“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
13 And the blood will be a sign on the houses where you are: when I see the blood I will go over you, and no evil will come on you for your destruction, when my hand is on the land of Egypt.
Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
14 And this day is to be kept in your memories: you are to keep it as a feast to the Lord through all your generations, as an order for ever.
“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
15 For seven days let your food be unleavened bread; from the first day no leaven is to be seen in your houses: whoever takes bread with leaven in it, from the first till the seventh day, will be cut off from Israel.
Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
16 And on the first day there is to be a holy meeting and on the seventh day a holy meeting; no sort of work may be done on those days but only to make ready what is necessary for everyone's food.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
17 So keep the feast of unleavened bread; for on this very day I have taken your armies out of the land of Egypt: this day, then, is to be kept through all your generations by an order for ever.
“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
18 In the first month, from the evening of the fourteenth day, let your food be unleavened bread till the evening of the twenty-first day of the month.
Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
19 For seven days no leaven is to be seen in your houses: for whoever takes bread which is leavened will be cut off from the people of Israel, if he is from another country or if he is an Israelite by birth.
Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
20 Take nothing which has leaven in it; wherever you are living let your food be unleavened cakes.
Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 Then Moses sent for the chiefs of Israel, and said to them, See that lambs are marked out for yourselves and your families, and let the Passover lamb be put to death.
Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
22 And take some hyssop and put it in the blood in the basin, touching the two sides and the top of the doorway with the blood from the basin; and let not one of you go out of his house till the morning.
Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
23 For the Lord will go through the land, sending death on the Egyptians; and when he sees the blood on the two sides and the top of the door, the Lord will go over your door and will not let death come in for your destruction.
Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
24 And you are to keep this as an order to you and to your sons for ever.
“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
25 And when you come into the land which the Lord will make yours, as he gave his word, you are to keep this act of worship.
Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
26 And when your children say to you, What is the reason of this act of worship?
Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
27 Then you will say, This is the offering of the Lord's Passover; for he went over the houses of the children of Israel in Egypt, when he sent death on the Egyptians, and kept our families safe. And the people gave worship with bent heads.
Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
28 And the children of Israel went and did so; as the Lord had given orders to Moses and Aaron, so they did.
Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
29 And in the middle of the night the Lord sent death on every first male child in the land of Egypt, from the child of Pharaoh on his seat of power to the child of the prisoner in the prison; and the first births of all the cattle.
Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
30 Then Pharaoh got up in the night, he and all his servants and all the Egyptians; and a great cry went up from Egypt; for there was not a house where someone was not dead.
Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
31 And he sent for Moses and Aaron by night, and said, Get up and go out from among my people, you and the children of Israel; go and give worship to the Lord as you have said.
Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
32 And take your flocks and your herds as you have said, and be gone; and give me your blessing.
Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
33 And the Egyptians were forcing the people on, to get them out of the land quickly; for they said, We are all dead men.
Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
34 And the people took their bread-paste before it was leavened, putting their basins in their clothing on their backs.
Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
35 And the children of Israel had done as Moses had said; and they got from the Egyptians ornaments of silver and of gold, and clothing:
Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
36 And the Lord had given the people grace in the eyes of the Egyptians so that they gave them whatever was requested. So they took away all their goods from the Egyptians.
Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
37 And the children of Israel made the journey from Rameses to Succoth; there were about six hundred thousand men on foot, as well as children.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
38 And a mixed band of people went with them; and flocks and herds in great numbers.
Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
39 And they made unleavened cakes from the paste which they had taken out of Egypt; it was not leavened, for they had been sent out of Egypt so quickly, that they had no time to make any food ready.
Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
40 Now the children of Israel had been living in Egypt for four hundred and thirty years.
Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
41 And at the end of four hundred and thirty years, to the very day, all the armies of the Lord went out of the land of Egypt.
Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
42 It is a watch-night before the Lord who took them out of the land of Egypt: this same night is a watch-night to the Lord for all the children of Israel, through all their generations.
Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
43 And the Lord said to Moses and Aaron, This is the law of the Passover: no man who is not an Israelite is to take of it:
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
44 But every man's servant, whom he has got for money, may take of it, when he has had circumcision.
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45 A man from a strange country living among you, and a servant working for payment, may not take part in it.
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46 It is to be taken in one house; not a bit of the flesh is to be taken out of the house, and no bone of it may be broken.
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47 All Israel is to keep the feast.
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48 And if a man from another country is living with you, and has a desire to keep the Passover to the Lord, let all the males of his family undergo circumcision, and then let him come near and keep it; for he will then be as one of your people; but no one without circumcision may keep it.
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49 The law is the same for him who is an Israelite by birth and for the man from a strange country who is living with you.
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 So the children of Israel did as the Lord gave orders to Moses and Aaron.
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51 And on that very day the Lord took the children of Israel out of the land of Egypt by their armies.
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.