< Ecclesiastes 12 >
1 Let your mind be turned to your Maker in the days of your strength, while the evil days come not, and the years are far away when you will say, I have no pleasure in them;
Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku za taabu, wala haijakaribia miaka utakaposema, “Mimi sifurahii hiyo”:
2 While the sun, or the light, or the moon, or the stars, are not dark, and the clouds come not back after the rain;
kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
3 In the day when the keepers of the house are shaking for fear, and the strong men are bent down, and the women who were crushing the grain are at rest because their number is small, and those looking out of the windows are unable to see;
siku ile walinzi wa nyumba watakapotetemeka, nao watu wenye nguvu watakapojiinamisha, wakati wasagao watakapokoma kwa sababu ya uchache, nao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
4 When the doors are shut in the street, and the sound of the crushing is low, and the voice of the bird is soft, and the daughters of music will be made low;
wakati milango ya kuingia barabarani itakapofungwa na sauti ya kusaga kufifia; wakati watu wataamshwa kwa sauti ya ndege, lakini nyimbo zao zote zikififia;
5 And he is in fear of that which is high, and danger is in the road, and the tree is white with flower, and the least thing is a weight, and desire is at an end, because man goes to his last resting-place, and those who are sorrowing are in the streets;
wakati watu watakapoogopa kilichoinuka juu na hatari zitakazokuwepo barabarani; wakati mlozi utakapochanua maua na panzi kujikokota nawe usiwe na shauku ya kitu chochote. Ndipo mwanadamu aiendea nyumba yake ya milele nao waombolezaji wakizunguka barabarani.
6 Before ever the silver cord is cut, or the vessel of gold is broken, or the pot is broken at the fountain, or the wheel broken at the water-hole;
Mkumbuke Muumba wako: kabla haijakatika kamba ya fedha, au bakuli la dhahabu halijavunjika; kabla mtungi kuvunjika kwenye chemchemi, au gurudumu kuvunjika kisimani,
7 And the dust goes back to the earth as it was, and the spirit goes back to God who gave it.
nayo mavumbi kurudi ardhini yalikotoka, na roho kurudi kwa Mungu aliyeitoa.
8 All things are to no purpose, says the Preacher, all is to no purpose.
Mhubiri asema, “Ubatili! Ubatili! Kila kitu ni ubatili!”
9 And because the Preacher was wise he still gave the people knowledge; searching out, testing, and putting in order a great number of wise sayings.
Mhubiri hakuwa tu na hekima, bali aliwagawia watu maarifa pia. Alitafakari na kutafiti na akaweka katika utaratibu mithali nyingi.
10 The Preacher made search for words which were pleasing, but his writing was in words upright and true.
Mhubiri alitafiti ili kupata maneno sahihi na kila alichoandika kilikuwa sawa na kweli.
11 The words of the wise are pointed, and sayings grouped together are like nails fixed with a hammer; they are given by one guide.
Maneno ya wenye hekima ni kama mchokoro, mithali zao zilizokusanywa pamoja ni kama misumari iliyogongomewa ikawa imara, yaliyotolewa na Mchungaji mmoja.
12 And further, my son, take note of this: of the making of books there is no end, and much learning is a weariness to the flesh.
Tena zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo, hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, nako kusoma sana huuchosha mwili.
13 This is the last word. All has been said. Have fear of God and keep his laws; because this is right for every man.
Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa: Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
14 God will be judge of every work, with every secret thing, good or evil.
Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au baya.