< Deuteronomy 5 >

1 And Moses sent for all Israel, and said to them, Give ear, O Israel, to the laws and the decisions which I give you today, and give attention to them so that you may keep and do them.
Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
2 The Lord our God made an agreement with us in Horeb.
Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
3 The Lord did not make this agreement with our fathers but with us, who are all living and present here today.
Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
4 The word of the Lord came to you face to face on the mountain, out of the heart of the fire,
Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
5 (I was between the Lord and you at that time, to make clear to you the word of the Lord: because, through fear of the fire, you did not go up the mountain; ) saying,
(Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
6 I am the Lord your God, who took you out of the land of Egypt, out of the prison-house.
“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
7 You are to have no other gods but me.
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
8 You may not make for yourselves an image in the form of anything in heaven or on earth or in the waters under the earth:
Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
9 You may not go down on your faces before them or give them worship: for I, the Lord your God, am a God who will not give his honour to another; and I will send punishment on the children for the wrongdoing of their fathers, to the third and fourth generation of my haters;
Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
10 And I will have mercy through a thousand generations on those who have love for me and keep my laws.
lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
11 You are not to make use of the name of the Lord your God for an evil purpose; whoever takes the Lord's name on his lips for an evil purpose will be judged as a sinner by the Lord.
Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
12 Keep the Sabbath day as a holy day, as you have been ordered by the Lord your God.
Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
13 On six days do all your work:
Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
14 But the seventh day is a Sabbath to the Lord your God; on that day do no work, you or your son or your daughter, or your man-servant or your woman-servant, or your ox or your ass or any of your cattle, or the man from a strange country who is living among you; so that your man-servant and your woman-servant may have rest as well as you.
Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
15 And keep in mind that you were a servant in the land of Egypt, and that the Lord your God took you out of that land by his strong hand and his stretched-out arm: for this reason the Lord has given you orders to keep the Sabbath day.
Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
16 Give honour to your father and your mother, as you have been ordered by the Lord your God; so that your life may be long and all may be well for you in the land which the Lord your God is giving you.
Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
17 Do not put anyone to death without cause.
Usiue.
18 Do not be false to the married relation.
Usizini.
19 Do not take the property of another.
Usiibe.
20 Do not give false witness against your neighbour;
Usimshuhudie jirani yako uongo.
21 Or let your desire be turned to your neighbour's wife, or his house or his field or his man-servant or his woman-servant or his ox or his ass or anything which is your neighbour's.
Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
22 These words the Lord said to all of you together on the mountain, out of the heart of the fire, out of the cloud and the dark, with a great voice: and he said no more; he put them in writing on the two stones of the law and gave them to me.
Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
23 And after hearing the voice which came out of the dark while the mountain was burning with fire, all the heads of your tribes and your chiefs came to me,
Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
24 And said, The Lord has let us see his glory and his power, and his voice has come to us out of the fire: today we have seen that a man may go on living even after hearing the voice of God.
Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
25 Why then is death to be our fate? For if the voice of the Lord our God comes to us any more, death will overtake us, and we will be burned up in this great fire.
Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
26 For what man is there in all the earth, who, hearing the voice of the living God as we have, out of the heart of the fire, has been kept from death?
Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
27 Do you go near: and after hearing everything which the Lord our God has to say, give us an account of all he has said to you, and we will give ear, and do it.
Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
28 Then the Lord, hearing your words to me, said to me, The words which this people have said to you have come to my ears: what they have said is well said.
Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
29 If only they had such a heart in them at all times, so that they might go in fear of me and keep my orders and that it might be well for them and for their children for ever!
Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
30 Now say to them, Go back to your tents.
“Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
31 But as for you, keep your place here by me, and I will give you all the orders and the laws and the decisions which you are to make clear to them, so that they may do them in the land which I am giving them for their heritage.
Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
32 Take care, then, to do whatever the Lord your God has given you orders to do; let there be no turning away to the right hand or to the left.
Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
33 Go on walking in the way ordered for you by the Lord your God, so that life may be yours and it may be well for you, and your days may be long in the land of your heritage.
Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.

< Deuteronomy 5 >