< Deuteronomy 25 >

1 If there is an argument between men and they go to law with one another, let the judges give their decision for the upright, and against the wrongdoer.
Iwapo kutakuwa na malumbano kati ya wanaume na wakaenda mahakamani, na waamuzi wakawahukumu, basi watamwachilia mtakatifu na kumhukumu muovu.
2 And if the wrongdoer is to undergo punishment by whipping, the judge will give orders for him to go down on his face and be whipped before him, the number of the blows being in relation to his crime.
Iwapo mwanamume mwenye hatia anastahili kupigwa, basi muamuzi atamfanya alale chini na kupigwa mbele zake kwa idadi iliyoamriwa kulingana na kosa lake.
3 He may be given forty blows, not more; for if more are given, your brother may be shamed before you.
Muamuzi anaweza kumpatia mapigo arobaini, lakini hapaswi kuvuka idadi hiyo; kwa maana akivuka idadi hiyo na kumpiga kwa mapigo mengi zaidi, basi Muisraeli mwenzako atakuwa kaaibishwa mbele ya macho yenu.
4 Do not keep the ox from taking the grain when he is crushing it.
Haupaswi kumfunga punda wako pua na mdomo anapokuwa akilima shamba lako.
5 If brothers are living together and one of them, at his death, has no son, the wife of the dead man is not to be married outside the family to another man: let her husband's brother go in to her and make her his wife, doing as it is right for a brother-in-law to do.
Iwapo kaka wanaishi pamoja na mmoja wao akafariki bila kuwa na mwana, basi mke wa marehemu hatakiwi kuolewa na mtu nje ya familia. Badala yake, kaka yake mumewe anapaswa kulala naye na kumchukua kuwa mke wake na kutekeleza wajibu wa kaka wa mume kwake.
6 Then the first male child she has will take the rights of the brother who is dead, so that his name may not come to an end in Israel.
Hii ni kwamba mtoto wa kwanza atakayezaliwa arithi chini ya jina la kaka yake mwanamume aliyefariki, ili jina lake lisiangamie ndani ya Israeli.
7 But if the man says he will not take his brother's wife, then let the wife go to the responsible men of the town, and say, My husband's brother will not keep his brother's name living in Israel; he will not do what it is right for a husband's brother to do.
Lakini kama mwanamume hataki kumchukua mke wa kaka yake awe wake, basi mke wa kaka yake anapaswa kwenda malangoni mpaka kwa wazee na kusema, “Kaka wa mume wangu amekataa kuwajibika kwa niaba ya jina la kaka yake humu Israeli; hataki kufanya wajibu wa kaka wa mume kwangu”.
8 Then the responsible men of the town will send for the man, and have talk with him: and if he still says, I will not take her;
Kisha wazee wa mji wake wanapaswa kumuita na kuzungumza naye. Lakini tuseme atasisitiza na kusema, “Sitaki kumchukua”.
9 Then his brother's wife is to come to him, before the responsible men of the town, and take his shoe off his foot, and put shame on him, and say, So let it be done to the man who will not take care of his brother's name.
Basi mke wa kaka yake anatakiwa kuja kwake mbele ya wazee, kumvua ndara zake miguuni mwake, na kumtemea usoni. Anapaswa kumjibu na kusema, “Hivi ndivyo kinachofanyika kwa mwanamume asiyetaka kujenga nyumba ya kaka yake”.
10 And his family will be named in Israel, The house of him whose shoe has been taken off.
Jina lake Israeli litaitwa, “Nyumba ya mtu aliyevuliwa ndara zake”.
11 If two men are fighting, and the wife of one of them, coming to the help of her husband, takes the other by the private parts;
Iwapo wanamume wamepigana wao kwa wao, na mke wa mmoja wao kaja kumkomboa mumewe dhidi ya yule aliyempiga, naye akanyosha mkono wake na kumshika sehemu za siri,
12 Her hand is to be cut off; have no pity on her.
basi unapaswa kuukata mkono yake; jicho lako halipaswi kuwa na huruma.
13 Do not have in your bag different weights, a great and a small;
Haupaswi kuwa na mizani ya uzito tofauti katika mfuko wako, mkubwa na mdogo.
14 Or in your house different measures, a great and a small.
Hautakiwi kuwa na vipimo tofauti ndani ya nyumba yako, vikubwa na vidogo.
15 But have a true weight and a true measure: so that your life may be long in the land which the Lord your God is giving you.
Unatakiwa kuwa na uzito kamili na wa haki; unatakiwa kuwa na vipimo kamili na vya haki, ili siku zako ziwe ndefu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia.
16 For all who do such things, and all whose ways are not upright, are disgusting to the Lord your God.
Kwa maana wote wanaofanya vitu hivi, wote wanaovunja haki, ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
17 Keep in mind what Amalek did to you on your way from Egypt;
Kumbuka ni jambo gani Amaleki alichofanya kwako barabarani ulipokuwa ukitoka Misri,
18 How, meeting you on the way, he made an attack on you when you were tired and without strength, cutting off all the feeble ones at the end of your line; and the fear of God was not in him.
jinsi alivyokutana na wewe barabarani na kuwashambulia kati yenu kwa nyuma, wale waliokuwa wamelegea nyuma, mlipokuwa dhaifu na kuchoka, hakumheshimu Mungu.
19 So when the Lord your God has given you rest from all who are against you on every side, in the land which the Lord your God is giving you for your heritage, see to it that the memory of Amalek is cut off from the earth; keep this in mind.
Kwa hiyo, Yahwe Mungu wako atakapowapa pumziko kutoka kwa maadui zako kila sehemu, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia kumiliki kama urithi, hautakiwi kusahau kuwa unapaswa kufuta kumbukumbu ya Waamaleki chini ya mbingu.

< Deuteronomy 25 >