< Deuteronomy 25 >

1 If there is an argument between men and they go to law with one another, let the judges give their decision for the upright, and against the wrongdoer.
Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.
2 And if the wrongdoer is to undergo punishment by whipping, the judge will give orders for him to go down on his face and be whipped before him, the number of the blows being in relation to his crime.
Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake,
3 He may be given forty blows, not more; for if more are given, your brother may be shamed before you.
lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.
4 Do not keep the ox from taking the grain when he is crushing it.
Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.
5 If brothers are living together and one of them, at his death, has no son, the wife of the dead man is not to be married outside the family to another man: let her husband's brother go in to her and make her his wife, doing as it is right for a brother-in-law to do.
Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.
6 Then the first male child she has will take the rights of the brother who is dead, so that his name may not come to an end in Israel.
Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.
7 But if the man says he will not take his brother's wife, then let the wife go to the responsible men of the town, and say, My husband's brother will not keep his brother's name living in Israel; he will not do what it is right for a husband's brother to do.
Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”
8 Then the responsible men of the town will send for the man, and have talk with him: and if he still says, I will not take her;
Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”
9 Then his brother's wife is to come to him, before the responsible men of the town, and take his shoe off his foot, and put shame on him, and say, So let it be done to the man who will not take care of his brother's name.
mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”
10 And his family will be named in Israel, The house of him whose shoe has been taken off.
Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.
11 If two men are fighting, and the wife of one of them, coming to the help of her husband, takes the other by the private parts;
Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,
12 Her hand is to be cut off; have no pity on her.
huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.
13 Do not have in your bag different weights, a great and a small;
Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.
14 Or in your house different measures, a great and a small.
Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.
15 But have a true weight and a true measure: so that your life may be long in the land which the Lord your God is giving you.
Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
16 For all who do such things, and all whose ways are not upright, are disgusting to the Lord your God.
Kwa maana Bwana Mungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.
17 Keep in mind what Amalek did to you on your way from Egypt;
Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.
18 How, meeting you on the way, he made an attack on you when you were tired and without strength, cutting off all the feeble ones at the end of your line; and the fear of God was not in him.
Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.
19 So when the Lord your God has given you rest from all who are against you on every side, in the land which the Lord your God is giving you for your heritage, see to it that the memory of Amalek is cut off from the earth; keep this in mind.
Bwana Mungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!

< Deuteronomy 25 >