< Daniel 5 >
1 Belshazzar the king made a great feast for a thousand of his lords, drinking wine before the thousand.
Mfalme Belshaza alifanya sherehe kubwa kwa kwa ajili ya wakuu wake wa kuheshimiwa wapatao elfu moja, na alikunywa divai mbele yao wote watu elfu moja.
2 Belshazzar, while he was overcome with wine, gave orders for them to put before him the gold and silver vessels which Nebuchadnezzar, his father, had taken from the Temple in Jerusalem; so that the king and his lords, his wives and his other women, might take their drink from them.
Wakati Belshaza alipokuwa akionja divai, alitoa agizo la kuleta vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu au kwa fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu huko Yerusalemu, ambavyo yeye, na wakuu wake, na wake zake, na masuria waliweza kuvinywea.
3 Then they took in the gold and silver vessels which had been in the Temple of the house of God at Jerusalem; and the king and his lords, his wives and his other women, took wine from them.
Watumishi walivileta vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu, nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Mfalme na wakuu wake, na wake zake na masuria walivinywea.
4 They took their wine and gave praise to the gods of gold and silver, of brass and iron and wood and stone.
Walikunywa divai na kuzisifu sanamu zao zilizotengenezwa kwa dhahabu na fedha, shaba, chuma, mbao na mawe.
5 In that very hour the fingers of a man's hand were seen, writing opposite the support for the light on the white wall of the king's house, and the king saw the part of the hand which was writing.
Kwa wakati huo huo vidole vya mkono wa mtu vilionekana mbele ya kinara cha taa na kuandika katika ukuta uliopigwa lipu katika ikulu ya mfalme. Mfalme aliweza kuona sehemu ya mkono ulipokuwa unaandika.
6 Then the colour went from the king's face, and he was troubled by his thoughts; strength went from his body, and his knees were shaking.
Ndipo uso wa mfalme ulibadilika na mawazo yake yalimwogopesha; miguu yake haikuweza kumfanya asimame, na magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja.
7 The king, crying out with a loud voice, said that the users of secret arts, the Chaldaeans, and the readers of signs, were to be sent for. The king made answer and said to the wise men of Babylon, Whoever is able to make out this writing, and make clear to me the sense of it, will be clothed in purple and have a chain of gold round his neck, and will be a ruler of high authority in the kingdom.
Mfalme alitoa agizo kwa kupiga kelele, waletwe ndani wale ambao hudai wanaweza kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wataalamu wa nyota. Mfalme akawaambia wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli, “Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. Naye atakuwa mtawala wa tatu wa juu kwa mamlaka katika ufalme.”
8 Then all the king's wise men came in: but they were not able to make out the writing or give the sense of it to the king.
Ndipo watu wote wa mfalme walikuwa wakijulikana kwa hekima yao waliingia ndani, lakini hawakuweza kuyasoma maandishi wala kueleza maana yake kwa mfalme.
9 Then King Belshazzar was greatly troubled and the colour went from his face, and his lords were at a loss.
Kisha mfalme Belshaza alishitushwa sana na mwonekano wa uso wake ulibadilika. Wakuu wake nao walishangazwa sana.
10 The queen, because of the words of the king and his lords, came into the house of the feast: the queen made answer and said, O King, have life for ever; do not be troubled by your thoughts or let the colour go from your face:
Ndipo sasa malkia alikuja katika nyumba ya sherehe kwasababu ya kile ambacho mfalme na wakuu wake walikuwa wamekisema. Malkia akasema, “Mfalme na aishi milele! Usiache mawazo yako yakakusumbua. Usiruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.
11 There is a man in your kingdom in whom is the spirit of the holy gods; and in the days of your father, light and reason like the wisdom of the gods were seen in him: and King Nebuchadnezzar, your father, made him master of the wonder-workers, and the users of secret arts, and the Chaldaeans, and the readers of signs;
Kuna mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu watakatifu dani yake. Katika siku za baba yako, mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake. Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme, alimfanya kuwa mkuu wa waganga, pamoja na mkuu wa wale wanazungumza na wafu, na wa wenye hekima, na wa wataalamu wa nyota.
12 Because a most special spirit, and knowledge and reason and the power of reading dreams and unfolding dark sayings and answering hard questions, were seen to be in him, even in Daniel (named Belteshazzar by the king): now let Daniel be sent for, and he will make clear the sense of the writing.
Roho bora, ufahamu, weledi, kutafsiri ndoto, kufafanua mafumbo na kutatua matatizo - hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Sasa mwiteni Danieli naye atawaambia maana ya kile kilichoandikwa.”
13 Then they took Daniel in before the king; the king made answer and said to Daniel, So you are that Daniel, of the prisoners of Judah, whom my father took out of Judah.
Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme. Mfalme akamwambia, “Wewe ni yule Danieli, mmoja kati ya watu wa mateka wa Yuda, ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda.
14 And I have had news of you, that the spirit of the gods is in you, and that light and reason and special wisdom have been seen in you.
Nimesikia habari kukuhusu wewe, kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na ya kwamba mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako.
15 And now the wise men, the users of secret arts, have been sent in before me for the purpose of reading this writing and making clear to me the sense of it: but they are not able to make clear the sense of the thing:
Na sasa watu wanaojulikana kwa hekima na wale wanaozungumza na wafu, wamekwisha kuletwa mbele yangu, ili kusoma maandishi haya na kunijulisha maana ya tafsiri yake, lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri yake.
16 And I have had news of you, that you have the power of making things clear, and of answering hard questions: now if you are able to make out the writing and give me the sense of it, you will be clothed in purple and have a gold chain round your neck and be a ruler of high authority in the kingdom.
Nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo. Sasa kama utaweza kusoma maandishi na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako, na utakuwa mtawala wa tatu mwenye mamlaka katika ufalme.”
17 Then Daniel made answer and said to the king, Keep your offerings for yourself, and give your rewards to another; but I, after reading the writing to the king, will give him the sense of it.
Kisha Danieli akajibu mbele ya mfalme, “Zawadi yako na iwe kwa ajili yako mwenyewe, na thawabu yako na umpe mtu mwingine. Hata hivyo, mfalme, nitakusomea maandishi na nitakwaambia maana.
18 As for you, O King, the Most High God gave to Nebuchadnezzar, your father, the kingdom and great power and glory and honour:
Na juu yako, Ewe mfalme, Mungu Aliye juu sana alimpa Nebukadneza baba yako ufalme, ukuu, heshima na enzi.
19 And because of the great power he gave him, all peoples and nations and languages were shaking in fear before him: some he put to death and others he kept living, at his pleasure, lifting up some and putting others down as it pleased him.
Na kwasababu ya ukuu huo, Mungu alimpa watu wote, mataifa, na lugha walimtetemekea na kumwogopa. Aliwauwa wale aliotaka wafe na aliwaacha hai wale aliotaka waishi. Aliwainua wale aliowataka, na aliwashusha wale aliowataka.
20 But when his heart was lifted up and his spirit became hard with pride, he was put down from his place as king, and they took his glory from him:
Lakini wakati moyo ulipokuwa na kiburi na roho yake ilifanywa kuwa mgumu na kwasababu hiyo alitenda kwa kiburi, alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme, na waliiondoa enzi yake.
21 And he was sent out from among the sons of men; and his heart was made like the beasts', and he was living with the asses of the fields; he had grass for his food like the oxen, and his body was wet with the dew of heaven, till he was certain that the Most High is ruler in the kingdom of men, and gives power over it to anyone at his pleasure.
Aliondolewa katika ubinadamu, alikuwa na akili za mnyama, na aliishi na punda wa mwituni. Alikula majani kama ng'ombe. Mwili wake ulilowanishwa kwa umande wa kutoka mbinguni mpaka pale alipojifunza kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na ya kwamba humweka mtu yeyote amtakaye juu yake.
22 And you, his son, O Belshazzar, have not kept your heart free from pride, though you had knowledge of all this;
Wewe mwana wake, Belshaza, haujaunyenyekeza moyo wako, ingawa aliyajua haya yote.
23 But you have been lifting yourself up against the Lord of heaven, and they have put the vessels of his house before you, and you and your lords, your wives and your women, have taken wine in them; and you have given praise to gods of silver and gold, of brass and iron and wood and stone, who are without the power of seeing or hearing, and without knowledge: and to the God in whose hand your breath is, and whose are all your ways, you have not given glory;
Umejiinua mwenyewe kinyume cha Bwana wa mbinguni. Katika nyumba yake walikuletea vyombo ambavyo wewe, wakuu wako, wake zako na masuria wako walivinywea, na kisha ukaisifia sana sanamu zilitengenezwa kwa fedha na dhahabu, shaba, chuma, mbao, na mawe - sanamu ambazo haziwezi kuona, kusikia wa kujua kitu chochote. Haujamheshimu Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake na ambaye anazijua njia zako zote.
24 Then the part of the hand was sent out from before him, and this writing was recorded.
Ndipo Mungu aliutuma mkono kutoka katika makao yake na maandishi haya yaliandikwa.
25 And this is the writing which was recorded, Mene, tekel, peres.
Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: 'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.'
26 This is the sense of the words: Mene; your kingdom has been numbered by God and ended.
Maana yake ni: 'Mene,' 'Mungu ameuhesabu ufalme wako na ameukomesha.'
27 Tekel; you have been put in the scales and seen to be under weight.
'Tekeli' 'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.'
28 Peres; your kingdom has been cut up and given to the Medes and Persians.
'Peresi' 'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'”
29 Then, by the order of Belshazzar, they put a purple robe on Daniel, and a gold chain round his neck, and a public statement was made that he was to be a ruler of high authority in the kingdom.
Ndipo Belshaza alitoa agizo, na walimvalisha Danieli mavazi ya zambarau. Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni, na mfalme alitoa tamko juu ya Danieli kuwa atakuwa mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu katika ufalme.
30 That very night Belshazzar, the king of the Chaldaeans, was put to death.
Usiku ule Belshaza, mfalme wa Babeli aliuawa,
31 And Darius the Mede took the kingdom, being then about sixty-two years old.
na Dario Mwajemi aliuchukua ufalme alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.