< Amos 5 >

1 Give ear to this word, my song of sorrow over you, O children of Israel.
Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:
2 The virgin of Israel has been made low, never again to be lifted up: she is stretched out by herself on her land; there is no one to put her on her feet again.
“Bikira Israeli ameanguka, kamwe hatainuka tena, ameachwa pweke katika nchi yake, hakuna yeyote wa kumwinua.”
3 For these are the words of the Lord God: The town which was able to send out a thousand, will have only a hundred; and that which sent out a hundred, will have only ten, in Israel.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli, mia moja tu watarudi; wakati mji utakapopeleka mia moja, kumi tu ndio watarudi hai.”
4 For these are the words of the Lord to the children of Israel: Let your hearts be turned to me, so that you may have life:
Hili ndilo Bwana asemalo kwa nyumba ya Israeli: “Nitafuteni mpate kuishi;
5 Do not be looking for help to Beth-el, and do not go to Gilgal, or make your way to Beer-sheba: for Gilgal will certainly be taken prisoner, and Beth-el will come to nothing.
msitafute Betheli, msiende Gilgali, msisafiri kwenda Beer-Sheba. Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni, na Betheli itafanywa kuwa si kitu.”
6 Go to the Lord for help so that you may have life; for fear that he may come like fire bursting out in the family of Joseph, causing destruction, and there will be no one to put it out in Beth-el.
Mtafuteni Bwana mpate kuishi, au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto; utawateketeza, nayo Betheli haitakuwa na yeyote wa kuuzima.
7 You who make the work of judging a bitter thing, crushing down righteousness to the earth;
Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu na kuiangusha haki chini
8 Go for help to him who makes Orion and the Pleiades, by whom the deep dark is turned into morning, who makes the day black with night; whose voice goes out to the waters of the sea, sending them out over the face of the earth: the Lord is his name;
(yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni, ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko na mchana kuwa usiku, ambaye huyaita maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake;
9 Who sends sudden destruction on the strong, so that destruction comes on the walled town.
yeye hufanya maangamizo kwenye ngome na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),
10 They have hate for him who makes protest against evil in the public place, and he whose words are upright is disgusting to them.
mnamchukia yule akemeaye mahakamani, na kumdharau yule ambaye husema kweli.
11 So because the poor man is crushed under your feet, and you take taxes from him of grain: you have made for yourselves houses of cut stone, but you will not take your rest in them; the fair vine-gardens planted by your hands will not give you wine.
Mnamgandamiza maskini na kumlazimisha awape nafaka. Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari, hamtaishi ndani yake; ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, hamtakunywa divai yake.
12 For I have seen how your evil-doing is increased and how strong are your sins, you troublers of the upright, who take rewards and do wrong to the cause of the poor in the public place.
Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu na ukubwa wa dhambi zenu. Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa na kuzuia haki ya maskini mahakamani.
13 So the wise will say nothing in that time; for it is an evil time.
Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.
14 Go after good and not evil, so that life may be yours: and so the Lord, the God of armies, will be with you, as you say.
Tafuteni mema, wala si mabaya, ili mpate kuishi. Ndipo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo yupo nanyi.
15 Be haters of evil and lovers of good, and let right be done in the public place: it may be that the Lord, the God of armies, will have mercy on the rest of Joseph.
Yachukieni maovu, yapendeni mema; dumisheni haki mahakamani. Yamkini Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atawahurumia mabaki ya Yosefu.
16 So these are the words of the Lord, the God of armies, the Lord: There will be weeping in all the open spaces; and in all the streets they will say, Sorrow! sorrow! and they will get in the farmer to the weeping, and the makers of sad songs to give cries of grief.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote na vilio vya uchungu katika njia kuu zote. Wakulima wataitwa kuja kulia, na waombolezaji waje kuomboleza.
17 In all the vine-gardens there will be cries of grief: for I will go through among you, says the Lord.
Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu, kwa kuwa nitapita katikati yenu,” asema Bwana.
18 Sorrow to you who are looking for the day of the Lord! what is the day of the Lord to you? it is dark and not light.
Ole wenu ninyi mnaoitamani siku ya Bwana! Kwa nini mnaitamani siku ya Bwana? Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.
19 As if a man, running away from a lion, came face to face with a bear; or went into the house and put his hand on the wall and got a bite from a snake.
Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba kumbe akakutana na dubu, kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta, kumbe akaumwa na nyoka.
20 Will not the day of the Lord be dark and not light? even very dark, with no light shining in it?
Je, siku ya Bwana haitakuwa giza, na si nuru: giza nene, bila mwonzi wa mwanga?
21 Your feasts are disgusting to me, I will have nothing to do with them; I will take no delight in your holy meetings.
“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22 Even if you give me your burned offerings and your meal offerings, I will not take pleasure in them: I will have nothing to do with the peace-offerings of your fat beasts.
Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
23 Take away from me the noise of your songs; my ears are shut to the melody of your instruments.
Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24 But let the right go rolling on like waters, and righteousness like an ever-flowing stream.
Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
25 Did you come to me with offerings of beasts and meal offerings in the waste land for forty years, O Israel?
“Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
26 Truly, you will take up Saccuth your king and Kaiwan your images, the star of your god, which you made for yourselves.
Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu, Sikuthi mungu wenu mtawala, na Kiuni mungu wenu wa nyota, ambao mliwatengeneza wenyewe.
27 And I will send you away as prisoners farther than Damascus, says the Lord, whose name is the God of armies.
Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,” asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.

< Amos 5 >