< 2 Chronicles 27 >

1 Jotham was twenty-five years old when he became king; and he was ruling in Jerusalem for sixteen years; and his mother's name was Jerushah, the daughter of Zadok.
Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
2 He did what was right in the eyes of the Lord, as his father Uzziah had done; but he did not go into the Temple of the Lord. And the people still went on in their evil ways.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
3 He put up the higher doorway of the house of the Lord, and did much building on the wall of the Ophel.
Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
4 In addition, he made towns in the hill-country of Judah, and strong buildings and towers in the woodlands.
Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
5 He went to war with the king of the children of Ammon and overcame them. That year, the children of Ammon gave him a hundred talents of silver, and ten thousand measures of grain and ten thousand measures of barley. And the children of Ammon gave him the same amount the second year and the third.
Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
6 So Jotham became strong, because in all his ways he made the Lord his guide.
Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
7 Now the rest of the acts of Jotham, and all his wars and his ways, are recorded in the book of the kings of Israel and Judah.
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 He was twenty-five years old when he became king, and he was ruling in Jerusalem for sixteen years.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
9 And Jotham went to rest with his fathers, and they put his body into the earth in the town of David; and Ahaz his son became king in his place.
Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chronicles 27 >