< 1 Samuel 24 >
1 Now when Saul came back from fighting the Philistines, news was given him that David was in the waste land of En-gedi.
Baada ya Sauli kurudi kuwafuatia Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika Jangwa la En-Gedi.”
2 Then Saul took three thousand of the best men out of all Israel, and went in search of David and his men on the rocks of the mountain goats.
Basi Sauli akachukua watu hodari 3,000 kutoka Israeli yote kwenda kumsaka Daudi na watu wake karibu na Majabali ya Mbuzi-Mwitu.
3 And on the way he came to a place where sheep were kept, where there was a hollow in the rock; and Saul went in for a private purpose. Now David and his men were in the deepest part of the hollow.
Akaja mpaka kwenye mazizi ya kondoo kando ya njia, hapo palikuwa na pango, na Sauli akaingia ndani kujipumzisha. Daudi na watu wake walikuwa wamo mle pangoni kwa ndani zaidi.
4 And David's men said to him, Now is the time when the Lord says to you, I will give up your hater into your hands to do with him whatever seems good to you. Then David, getting up, took the skirt of Saul's robe in his hand, cutting off the end of it without his knowledge.
Watu wa Daudi wakasema, “Hii ndiyo siku aliyonena Bwana akikuambia, ‘Nitamtia adui yako mikononi mwako ili wewe umtendee utakavyo.’” Basi Daudi akanyemelea bila kuonekana na kukata upindo wa joho la Sauli.
5 And later, David was full of regret for cutting off Saul's skirt.
Baada ya hilo, dhamiri ya Daudi ikataabika kwa kukata upindo wa joho la Sauli.
6 And David said to his men, Before the Lord, never let it be said that my hand was lifted up against my lord, the man of the Lord's selection, for the Lord's holy oil has been put on him.
Akawaambia watu wake, “Bwana na apishie mbali nisije nikafanya jambo kama hilo kwa bwana wangu, yeye ambaye ni mpakwa mafuta wa Bwana, au kuinua mkono wangu dhidi yake; kwani yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.”
7 So with these words David kept his servants back, and did not let them make an attack on Saul. And Saul got up and went on his way.
Kwa maneno haya Daudi akawaonya watu wake na hakuwaruhusu wamshambulie Sauli. Naye Sauli akaondoka pangoni na kwenda zake.
8 And after that David came out of the hollow rock, and crying after Saul said, My lord the king. And when Saul gave a look back, David went down on his face and gave him honour.
Ndipo Daudi naye akatoka pangoni na kumwita Sauli akisema, “Mfalme, bwana wangu!” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama na kusujudu uso wake mpaka nchi.
9 And David said to Saul, Why do you give any attention to those who say that it is my desire to do you wrong?
Akamwambia Sauli, “Kwa nini unasikiliza wakati watu wanapokuambia, ‘Daudi amenuia kukudhuru’?
10 Look! you have seen today how the Lord gave you up into my hands even now in the hollow of the rocks: and some would have had me put you to death, but I had pity on you: for I said, Never will my hand be lifted up against my lord, who has been marked with the holy oil.
Leo umeona kwa macho yako mwenyewe jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu huko pangoni. Watu wengine walisisitiza nikuue, lakini nilikuacha, nikisema, ‘Sitainua mkono wangu dhidi ya bwana wangu, kwa sababu yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.’
11 And see, my father, see the skirt of your robe in my hand: for the fact that I took off the skirt of your robe and did not put you to death is witness that I have no evil purpose, and I have done you no wrong, though you are waiting for my life to take it.
Tazama, baba yangu, ona kipande hiki cha joho lako mkononi mwangu! Nilikata upindo wa joho lako lakini sikukuua. Basi ujue na kutambua kuwa sina hatia ya kutenda mabaya wala ya kuasi. Wewe sijakukosea, lakini wewe unaniwinda mimi ili kuuondoa uhai wangu.
12 May the Lord be judge between me and you, and may the Lord give me my rights against you, but my hand will never be lifted up against you.
Bwana na ahukumu kati yangu na wewe. Naye Bwana alipize mabaya unayonitendea, lakini mkono wangu hautakugusa.
13 There is an old saying, From the evil-doer comes evil: but my hand will never be lifted up against you.
Kama msemo wa kale usemavyo, ‘Kutoka kwa watenda maovu hutoka matendo maovu,’ kwa hiyo mkono wangu hautakugusa wewe.
14 After whom has the king of Israel come out? for whom are you searching? for a dead dog, an insect.
“Je, mfalme wa Israeli ametoka dhidi ya nani? Ni nani unayemfuatia? Je, ni mbwa mfu? Ni kiroboto?
15 So let the Lord be judge, and give a decision between me and you, and see and give support to my cause, and keep me from falling into your hands.
Bwana na awe mwamuzi wetu, yeye na aamue kati yetu. Yeye na anitetee shauri langu; anihesabie haki kwa kuniokoa mkononi mwako.”
16 Now when David had said these words to Saul, Saul said, Is this your voice, David, my son? And Saul was overcome with weeping.
Daudi alipomaliza kusema haya, Sauli akamuuliza, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Ndipo Sauli akalia kwa sauti kuu, akisema,
17 And he said to David, You are right and I am wrong: for you have given me back good, but I have given you evil.
“Wewe ni mwenye haki kuliko mimi; umenitendea mema, lakini mimi nimekutendea mabaya.
18 And you have made clear to me how good you have been to me today: because, when the Lord gave me up into your hands, you did not put me to death.
Sasa umeniambia juu ya mema uliyonitendea. Bwana alinitia mikononi mwako, lakini wewe hukuniua.
19 If a man comes across his hater, will he let him get away safe? so may you be rewarded by the Lord for what you have done for me today.
Je, mtu ampatapo adui yake, humwacha aende zake bila kumdhuru? Bwana na akulipe mema kwa jinsi ulivyonitenda leo.
20 And now I am certain that you will be king, and that the kingdom of Israel will be made strong under your authority.
Ninajua kwamba hakika utakuwa mfalme na ya kwamba ufalme wa Israeli utakuwa imara mikononi mwako.
21 So give me your oath by the Lord, that you will not put an end to my seed after me or let my name be cut off from my father's family.
Sasa niapie kwa Bwana kwamba hutakatilia mbali uzao wangu wala kulifuta jina langu kutoka jamaa ya baba yangu.”
22 And David gave Saul his oath. And Saul went back to his house; but David and his men went up to their safe place.
Basi Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akarudi zake nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.