< 1 Kings 2 >

1 Now the time of David's death came near; and he gave orders to Solomon his son, saying,
Daudi alipokaribia kufa, alimwamuru Sulemani mwanae, akisema,
2 I am going the way of all the earth: so be strong and be a man;
“Mimi sasa ninaiendea njia ya dunia yote. Kwa hiyo, uwe imara, na ujionyeshe mwenyewe kama mwanamume. Uzilinde amri za BWANA, Mungu wako ukitembea katika njia zake, utii maaagizo yake, amari zake,
3 And keep the orders of the Lord your God, walking in his ways, keeping his laws and his orders and his rules and his words, as they are recorded in the law of Moses; so that you may do well in all you do and wherever you go,
maamuzi yake, na maagizo ya maagano yake, uwe mwamngalifu kufanya yale yaliyoandikwa katika sheria za Musa, ili ufanikiwe katika yote utakayoyafanya, popote kule utakakokuwa,
4 So that the Lord may give effect to what he said of me, If your children give attention to their ways, living uprightly before me with all their heart and their soul, you will never be without a man to be king in Israel.
na BWANA atayatimiza maneno yake aliyosema kuhusu mimi, aliposema, 'kama wanao watajilinda katika tabia zao, wakatembea mbele yangu kwa uaminifu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, hawatakoma kuwa na mtu aliyeketi katika kiti cha enzi cha Israeli.
5 Now you have knowledge of what Joab, the son of Zeruiah, did to me, and to the two captains of the army of Israel, Abner, the son of Ner, and Amasa, the son of Jether, whom he put to death, taking payment for the blood of war in time of peace, and making the band of my clothing and the shoes on my feet red with the blood of one put to death without cause.
Wewe pia wajua kile Yoabu mwana wa Seruya alichonifanyia, na kile alichowafnyia majemedari wa majeshi y a Israeli, kwa Abina mwana wa Neri, na kwa Amasa mwana wa Yetheri, ambaye alimwua. Alimwaga damu vitani wakati wa amani na kuiweka ile damu kwenye mshipi uliokuwa kiunoni mwake na kwenye vile viatu miguuni mwake.
6 So be guided by your wisdom, and let not his white head go down to the underworld in peace. (Sheol h7585)
Mshughulikie Yoabu kwa hekima ambayo umejifunza, lakini usiache mvi zake ziingie kaburini kwa amani. (Sheol h7585)
7 But be good to the sons of Barzillai the Gileadite, and let them be guests at your table; for so they came to me when I went in flight from Absalom your brother.
Hata hivyo, uonyeshe utu kwa wana wa Barizilai Mgileadi, na uwaache wawe miongoni mwa wale wanaokula mezani kwako, kwa kuwa walikuja kwangu wakati nilipomkimbia ndugu yangu Absalomu.
8 Now you have with you Shimei, the son of Gera the Benjamite of Bahurim, who put a bitter curse on me on the day when I went to Mahanaim; but he came down to see me at Jordan, and I gave him my oath by the Lord, saying, I will not put you to death by the sword.
Tazama, Shimei mwana wa Gera yuko pamoja na wewe, Wabenjamini wa Bahurimu, walionilaani kwa laana ya fujo siku niliyoenda kwa Mahanaimu. Shimei alishuka kuja kuniona pale Yorodani, na nikamwapia kwa BWANA, nikisema, 'Sitawaua kwa upanga,'
9 But do not let him be free from punishment, for you are a wise man; and it will be clear to you what you have to do with him; see that his white head goes down to the underworld in blood. (Sheol h7585)
Kwa hiyo sasa usimwache aiepuke adhabu. Wewe ni mwenye hekima, na utajua jinsi itakavyokupasa kumtendea. Utakileta hicho kichwa chenye mvi chini kaburini.” (Sheol h7585)
10 Then David went to rest with his fathers, and his body was put into the earth in the town of David.
Ndipo Daudi alipolala na mababu zake na alizikwa kwenye mji wa Daudi.
11 David was king over Israel for forty years: for seven years he was king in Hebron and for thirty-three years in Jerusalem.
Siku ambazo Daudi alitwala Israeli zilikuwani miaka arobaini. Alikuwa ametawala kwa miaka saba kule Hebroni na kwa miaka thelethini na tatu kule Yerusalemu.
12 And Solomon took his place on the seat of David his father, and his kingdom was made safe and strong.
Kisha Sulemani akaketi kwenye kiti cha enzi cha baba yake Daudi, na utawala wake ulikuwa imara.
13 Then Adonijah, the son of Haggith, came to Bath-sheba, the mother of Solomon. And she said, Come you in peace? And he said, Yes, in peace.
Kisha Adoniya mwana wa Hagathi alikuja kwa Bathisheba mama wa Sulemani., Naye akamwuliza, “Je, unakuja kwa amani?” Naye akajiibu. “kwa amani.”
14 Then he said, I have something to say to you. And she said, Say on.
Kisha akasema, “Nina jambo la kukuambia.” Naye akajibu, “Sema.”
15 And he said, You saw how the kingdom was mine, and all Israel had the idea that I would be their king; but now the kingdom is turned about, and has become my brother's, for it was given to him by the Lord.
Adoniya amesema, “Unajua kuwa ufalme ulikuwa wangu, na kwamba Israeli yote ilikuwa inanitegemea mimi kuwa mfalme. Hata hivyo, ufalme umegeuzwa na umekuwa wa ndugu yangu, kwani ulikuwa wake toka kwa BWANA.
16 Now I have one request to make to you, and do not say, No, to me. And she said to him, Say on.
Sasa nina ombi moja kwako. Usinikatalie.”Bathisheba akamwambia, “Sema.”
17 Then he said, Will you go to Solomon the king (for he will not say, No, to you) and put before him my request that he will give me Abishag the Shunammite for a wife?
Naye akamwambia, “Tafadhali mwambie mfalme Sulemani, kwa kuwa hatakukatalia, ili kwamba anipatie Abishagi Mshunami awe mke wangu.”
18 And Bath-sheba said, Good! I will make your request to the king.
Bathisheba akamwambia, “Vyema sana, nitamwambia mfalme”
19 So Bath-sheba went to King Solomon to have talk with him on Adonijah's account. And the king got up to come to her, and went down low to the earth before her; then he took his place on the king's seat and had a seat made ready for the king's mother and she took her place at his right hand.
Kwa hiyo Bathisheba akaenda kumwambia, mfalme Sulemani kwa niaba ya Adoniya. Mfalme akainuka kumlaki na akapiga magoti mbele yake. Kisha akaa kwenye kiti chake cha enzi na kulikuwa na kiti kingine cha enzi kilicholetwa kwa ajili ya mama wa mfalme. Naye akaa mkono wa kuume wa mfalme.
20 Then she said, I have one small request to make to you; do not say, No, to me. And the king said, Say on, my mother, for I will not say, No, to you.
Ndipo alipomwambia, “Napenda kukuomba ombi moja dogo. Usinikalie.” Mfalme, akamjibu, “Mama omba kwa kuwa sitakukatalia.”
21 And she said, Let Abishag the Shunammite be given to Adonijah your brother for a wife.
Naya akamwambia, “Naomba Abishagi Mshunami apewe Adoniya ndugu yako awe mke wake.”
22 Then King Solomon made answer and said to his mother, Why are you requesting me to give Abishag the Shunammite to Adonijah? Take the kingdom for him in addition, for he is my older brother, and Abiathar the priest and Joab, the son of Zeruiah, are on his side.
Mfalme Sulemani akamjibu mama yake, “Kwa nini unamwombea Adoniya huyo Abishagi Mshunami? Kwa nini usimwombee ufalme pia, kwa kuwa ni ndugu yangu mkubwa? - au kwa Abiathari kuhani, au Yoabu mwana wa Seruya?”
23 Then King Solomon took an oath by the Lord, saying, May God's punishment be on me if Adonijah does not give payment for these words with his life.
Kisha mfalme Sulemani akaapa kwa BWANA, akisema, “Mungu wangu na anifanyie hivyo, na zaidi pia, kama Adoniya hajayasema haya kinyume na maisha yake.
24 Now by the living Lord, who has given me my place on the seat of David my father, and made me one of a line of kings, as he gave me his word, truly Adonijah will be put to death this day.
Sasa basi kama BWANA aishivyo, ambaye ndiye alinifanya mimi kuwepo na kunipa kiti cha enzi cha Daudi baba yangu, na ambaye amenifanyia nyumba kwa ahadi yake, hakika Adoniya lazima auawe leo.”
25 And King Solomon sent Benaiah, the son of Jehoiada, and he made an attack on him and put him to death.
Kwa hiyo mfalme Sulemani akamtuma Benaya mwana wa Yehoyada naye akamkuta Adoniya na kumwua.
26 And to Abiathar the priest the king said, Go to Anathoth, to your fields; for death would be your right reward; but I will not put you to death now, because you took up the ark of the Lord God before David my father, and you were with him in all his troubles.
Kisha akamwambia Abiathari kuhani, “Nenda kwa Anathothi, kwenye mashamba yako. unastahili kufa, lakini sitakua sasa hivi, kwa sababu ulilbeba sanduku la BWANA mbele ya Daudi baba yangu na kujitabisha kwa namna mbalimbali kama baba yangu alivyopata tabu.”
27 So Solomon let Abiathar be priest no longer, so that he might make the word of the Lord come true which he said about the sons of Eli in Shiloh.
Kwa hiyo Sulemani akamfukuza Abiathari asiwe kuhani wa BWANA, ili kwamba atimilize maneno ya BWANA, aliyokuwa amesema juu ya nyumba ya Eli.
28 And news of this came to Joab; for Joab had been one of Adonijah's supporters, though he had not been on Absalom's side. Then Joab went in flight to the Tent of the Lord, and put his hands on the horns of the altar.
Habari hizo zikamfikia Yoabu, Kwani Yoabu alimuunga mkono Adoniya, ingawa hakumuunga mkono Absalomu. Kwa hiyo Yoabu akakimbilia kwenye hema ya BWANA karibu na madhabahu na akabeba pembe za madhabahu.
29 And they said to King Solomon, Joab has gone in flight to the Tent of the Lord and is by the altar. Then Solomon sent Benaiah, the son of Jehoiada, saying, Go, make an attack on him.
Sulemani alipoambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema ya BWANA na sasa alikuwa karibu na madhabahu. Ndipo Sulemani alipomtuma Benaya mwana wa Yehoyada, akisema, “Nenda, ukamwue.”
30 And Benaiah came to the Tent of the Lord and said to him, The king says, Come out. And he said, No; but let death come to me here. And Benaiah went back to the king and gave him word of the answer which Joab had given.
Kwa hiyo Benaya akaenda kwenye hema ya BWANA na kumwambia, “Mfalme anasema utoke hemani.” Yoabu akamjibu, “Hapana, Nitafia hapa,” Kwa hiyo Benaya akarudi kwa mfalme, akasema, “Yoabu amesema atafia kwenye madhabahu,”
31 And the king said, Do as he has said and make an attack on him there, and put his body into the earth; so that you may take away from me and from my family the blood of one put to death by Joab without cause.
Naye mfalme akamwambia, “Kafanye kama alivyosema. Muue na ukamzike, ili kwamba uitoe kwangu na kwenye nyumba ya baba yangu damu ambayo Yoabu alimwaga bila sababu.
32 And the Lord will send back his blood on his head, because of the attack he made on two men more upright and better than himself, putting them to the sword without my father's knowledge; even Abner, the son of Ner, captain of the army of Israel, and Amasa, the son of Jether, captain of the army of Judah.
BWANA na amrudishie damu yake kichwani kwake, kwa sababu aliwaua wanaume wawili wasio na hatia na wema kuliko yeye na akawaua kwa upanga, Abineri mwana wa Neri, Jemedari wa Jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Jetheri, jemedari wa jeshi la Yuda, bila baba yangu Daudi kujua.
33 So their blood will be on the head of Joab, and on the head of his seed for ever; but for David and his seed and his family and the seat of his kingdom, there will be peace for ever from the Lord.
Kwa hiyo damu yao na imrudie Yoabu kichwani pake na kwenye vichwa vya uzao wake milele na milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, na nyumba yake, na kwenye kiti chake cha enzi, kuwe na amani ya kudumu kutoka kwa BWANA.”
34 So Benaiah, the son of Jehoiada, went up, and falling on him, put him to death; and his body was put to rest in his house in the waste land.
Kisha Benaya mwana wa Yehoyada akaenda akamvamia Yoabu na kumwua. Alizikwa kwenye nyumba yake kule jangwani.
35 And the king put Benaiah, the son of Jehoiada, in his place over the army; and Zadok the priest he put in the place of Abiathar.
Mfalme akamwinua Benaya mwana wa Yehoyada kuwa juu ya jeshi badala yake, na akamweka Sadoki kuhani kwenye nafasi ya Abiatahari.
36 Then the king sent for Shimei, and said to him, Make a house for yourself in Jerusalem and keep there and go to no other place.
Kisha Mfalme akatuma watu kumwita Shimei, na akamwambia, “Kajijengee nyumba kwa ajili yako kule Yerusalemu na ushi huko, na usitoke nje ya Huo mji na kwenda mahali pengine.
37 For be certain that on the day when you go out and go over the stream Kidron, death will overtake you: and your blood will be on your head.
Kwa kuwa siku utakayoenda mahali pengine, na kupita bonde la Kidroni, ujue kwa hakika kuwa utakufa. Damu yako itakuwa juu ya kichwa chako.”
38 And Shimei said to the king, Very well! as my lord the king has said, so will your servant do. And for a long time Shimei went on living in Jerusalem.
Kwa hiyo Shimei akamwambia mfalme, “Unachosema ni chema. Kama vike mfalme bwana wangu alivyosema, ndivyo ambavyo mtumishi wako atakavyofanya.” Kwa hiyo Shimei akaishi Yerusalemu kwa miaka mingi.
39 But after three years, two of the servants of Shimei went in flight to Achish, son of Maacah, king of Gath. And word was given to Shimei that his servants had gone to Gath.
Lakiini mwishoni mwa mwaka wa tatu, watumishi wawili wa Shimei wakakimbilia kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi. Kwa hiyo wakamwambia Shimei, wakisema, “Tazama, watumishi wako wameenda Gathi,”
40 Then Shimei got up, and making ready his ass, he went to Gath, to Achish, in search of his servants; and he sent and got them from Gath.
Kisha Shimei akainuka, akapanda punda wake akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumishi wake. Akaenda na akawaleta watumishi wake toka Gathi.
41 And news was given to Solomon that Shimei had gone from Jerusalem to Gath and had come back again.
Sulemani alipoambiwa kuwa Shimei alikuwa ametoka Yerusalemu kwenda Gathi na amerudi,
42 Then the king sent for Shimei, and said to him, Did I not make you take an oath by the Lord, protesting to you and saying, Be certain that on the day when you go out from here, wherever you go, death will overtake you? and you said to me, Very well!
mfalme akatuma wito kwa Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapisha kwa BWANA na kushuhudia kwako, nikisema, 'Tambua kuwa siku utakayotoka kwenda nje na kwenda mahali popote, hakika utakufa'? Na ukaniambia kuwa unachosema ni chema.'
43 Why then have you not kept the oath of the Lord and the order which I gave you?
Kwa nini basi umeshindwa kulinda kiapo chako kwa BWANA na amri niliyokupa?”
44 And the king said to Shimei, You have knowledge of all the evil which you did to David my father; and now the Lord has sent back your evil on yourself.
Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako maovu yote uliyofanya kwa baba yangu Daudi. Kwa hiyo BWANA atakurudishia maovu yako kichwani pako.
45 But a blessing will be on King Solomon, and the kingdom of David will keep its place before the Lord for ever.
Lakini Sulemani atabarikiwa na enzi ya Daudi itaimarika mbele ya BWANA milele.”
46 So the king gave orders to Benaiah, the son of Jehoiada; and he went out and, falling on him, put him to death. And Solomon's authority over the kingdom was complete.
Kwa hiyo mfalme akamwamuru Benaya mwana wa Yehoyada kwenda kumwua Shimei. Kwa hiyo ule utawala ulikuwa mwema kwa mkono wa Sulemain.

< 1 Kings 2 >