< Psalms 88 >

1 A song. A Psalm of the sons of Korah. For the choirmaster. According to Mahalath Leannoth. A Maskil of Heman the Ezrahite. O LORD, the God of my salvation, day and night I cry out before You.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 May my prayer come before You; incline Your ear to my cry.
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 For my soul is full of troubles, and my life draws near to Sheol. (Sheol h7585)
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
4 I am counted among those descending to the Pit. I am like a man without strength.
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 I am forsaken among the dead, like the slain who lie in the grave, whom You remember no more, who are cut off from Your care.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 You have laid me in the lowest Pit, in the darkest of the depths.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Your wrath weighs heavily upon me; all Your waves have submerged me.
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 You have removed my friends from me; You have made me repulsive to them; I am confined and cannot escape.
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 My eyes grow dim with grief. I call to You daily, O LORD; I spread out my hands to You.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 Do You work wonders for the dead? Do departed spirits rise up to praise You?
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 Can Your loving devotion be proclaimed in the grave, Your faithfulness in Abaddon?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 Will Your wonders be known in the darkness, or Your righteousness in the land of oblivion?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 But to You, O LORD, I cry for help; in the morning my prayer comes before You.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 Why, O LORD, do You reject me? Why do You hide Your face from me?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 From my youth I was afflicted and near death. I have borne Your terrors; I am in despair.
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 Your wrath has swept over me; Your terrors have destroyed me.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 All day long they engulf me like water; they enclose me on every side.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 You have removed my beloved and my friend; darkness is my closest companion.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

< Psalms 88 >