< Psalms 78 >

1 A Maskil of Asaph. Give ear, O my people, to my instruction; listen to the words of my mouth.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I will open my mouth in parables; I will utter things hidden from the beginning,
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 that we have heard and known and our fathers have relayed to us.
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 We will not hide them from their children, but will declare to the next generation the praises of the LORD and His might, and the wonders He has performed.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 For He established a testimony in Jacob and appointed a law in Israel, which He commanded our fathers to teach to their children,
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 that the coming generation would know them— even children yet to be born— to arise and tell their own children
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 that they should put their confidence in God, not forgetting His works, but keeping His commandments.
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 Then they will not be like their fathers, a stubborn and rebellious generation, whose heart was not loyal, whose spirit was not faithful to God.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 The archers of Ephraim turned back on the day of battle.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 They failed to keep God’s covenant and refused to live by His law.
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 They forgot what He had done, the wonders He had shown them.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 He worked wonders before their fathers in the land of Egypt, in the region of Zoan.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 He split the sea and brought them through; He set the waters upright like a wall.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 He led them with a cloud by day and with a light of fire all night.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 He split the rocks in the wilderness and gave them drink as abundant as the seas.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 He brought streams from the stone and made water flow down like rivers.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 But they continued to sin against Him, rebelling in the desert against the Most High.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 They willfully tested God by demanding the food they craved.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 They spoke against God, saying, “Can God really prepare a table in the wilderness?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 When He struck the rock, water gushed out and torrents raged. But can He also give bread or supply His people with meat?”
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Therefore the LORD heard and was filled with wrath; so a fire was kindled against Jacob, and His anger flared against Israel,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 because they did not believe God or rely on His salvation.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Yet He commanded the clouds above and opened the doors of the heavens.
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 He rained down manna for them to eat; He gave them grain from heaven.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Man ate the bread of angels; He sent them food in abundance.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 He stirred the east wind from the heavens and drove the south wind by His might.
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 He rained meat on them like dust, and winged birds like the sand of the sea.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 He felled them in the midst of their camp, all around their dwellings.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 So they ate and were well filled, for He gave them what they craved.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Yet before they had filled their desire, with the food still in their mouths,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 God’s anger flared against them, and He put to death their strongest and subdued the young men of Israel.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 In spite of all this, they kept on sinning; despite His wonderful works, they did not believe.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 So He ended their days in futility, and their years in sudden terror.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 When He slew them, they would seek Him; they repented and searched for God.
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 And they remembered that God was their Rock, that God Most High was their Redeemer.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 But they deceived Him with their mouths, and lied to Him with their tongues.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Their hearts were disloyal to Him, and they were unfaithful to His covenant.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 And yet He was compassionate; He forgave their iniquity and did not destroy them. He often restrained His anger and did not unleash His full wrath.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 He remembered that they were but flesh, a passing breeze that does not return.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 How often they disobeyed Him in the wilderness and grieved Him in the desert!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Again and again they tested God and provoked the Holy One of Israel.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 They did not remember His power — the day He redeemed them from the adversary,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 when He performed His signs in Egypt and His wonders in the fields of Zoan.
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 He turned their rivers to blood, and from their streams they could not drink.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 He sent swarms of flies that devoured them, and frogs that devastated them.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 He gave their crops to the grasshopper, the fruit of their labor to the locust.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 He killed their vines with hailstones and their sycamore-figs with sleet.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 He abandoned their cattle to the hail and their livestock to bolts of lightning.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 He unleashed His fury against them, wrath, indignation, and calamity— a band of destroying angels.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 He cleared a path for His anger; He did not spare them from death but delivered their lives to the plague.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 He struck all the firstborn of Egypt, the virility in the tents of Ham.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 He led out His people like sheep and guided them like a flock in the wilderness.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 He led them safely, so they did not fear, but the sea engulfed their enemies.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 He brought them to His holy land, to the mountain His right hand had acquired.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 He drove out nations before them and apportioned their inheritance; He settled the tribes of Israel in their tents.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 But they tested and disobeyed God Most High, for they did not keep His decrees.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 They turned back and were faithless like their fathers, twisted like a faulty bow.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 They enraged Him with their high places and provoked His jealousy with their idols.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 On hearing it, God was furious and rejected Israel completely.
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 He abandoned the tabernacle of Shiloh, the tent He had pitched among men.
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 He delivered His strength to captivity, and His splendor to the hand of the adversary.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 He surrendered His people to the sword because He was enraged by His heritage.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Fire consumed His young men, and their maidens were left without wedding songs.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 His priests fell by the sword, but their widows could not lament.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Then the Lord awoke as from sleep, like a mighty warrior overcome by wine.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 He beat back His foes; He put them to everlasting shame.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 He rejected the tent of Joseph and refused the tribe of Ephraim.
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 But He chose the tribe of Judah, Mount Zion, which He loved.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 He built His sanctuary like the heights, like the earth He has established forever.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 He chose David His servant and took him from the sheepfolds;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 from tending the ewes He brought him to be shepherd of His people Jacob, of Israel His inheritance.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 So David shepherded them with integrity of heart and guided them with skillful hands.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

< Psalms 78 >