< Psalms 59 >
1 For the choirmaster. To the tune of “Do Not Destroy.” A Miktam of David, when Saul sent men to watch David’s house in order to kill him. Deliver me from my enemies, O my God; protect me from those who rise against me.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
2 Deliver me from workers of iniquity, and save me from men of bloodshed.
Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
3 See how they lie in wait for me. Fierce men conspire against me for no transgression or sin of my own, O LORD.
Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
4 For no fault of my own, they move swiftly to attack me. Arise to help me, and take notice.
Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
5 O LORD God of Hosts, the God of Israel, rouse Yourself to punish all the nations; show no mercy to the wicked traitors.
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
6 They return in the evening, snarling like dogs and prowling around the city.
Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
7 See what they spew from their mouths— sharp words from their lips: “For who can hear us?”
Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
8 But You, O LORD, laugh at them; You scoff at all the nations.
Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
9 I will keep watch for You, O my strength, because You, O God, are my fortress.
Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
10 My God of loving devotion will come to meet me; God will let me stare down my foes.
Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
11 Do not kill them, or my people will forget. Scatter them by Your power, and bring them down, O Lord, our shield.
Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
12 By the sins of their mouths and the words of their lips, let them be trapped in their pride, in the curses and lies they utter.
Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
13 Consume them in wrath; consume them till they are no more, so it may be known to the ends of the earth that God rules over Jacob.
wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
14 They return in the evening, snarling like dogs and prowling around the city.
Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
15 They scavenge for food, and growl if they are not satisfied.
Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
16 But I will sing of Your strength and proclaim Your loving devotion in the morning. For You are my fortress, my refuge in times of trouble.
Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
17 To You, O my strength, I sing praises, for You, O God, are my fortress, my God of loving devotion.
Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.