< Psalms 57 >

1 For the choirmaster. To the tune of “Do Not Destroy.” A Miktam of David, when he fled from Saul into the cave. Have mercy on me, O God, have mercy, for in You my soul takes refuge. In the shadow of Your wings I will take shelter until the danger has passed.
Unihurumie, Mungu, unihurumie mimi, kwa maana ninakukimbilia wewe mpaka matatizo haya yaishe. Ninakaa chini ya mbawa za zako kwa ajili ya ulinzi mpaka huu uharibifu utakapoisha.
2 I cry out to God Most High, to God who fulfills His purpose for me.
Nitakulilia Mungu uliye hai, kwa Mungu, afanyaye mambo yote kwa ajili yangu.
3 He reaches down from heaven and saves me; He rebukes those who trample me. (Selah) God sends forth His loving devotion and His truth.
Yeye atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa, ana hasira na wale wanaonishambulia. (Selah) Mungu atanitumia upendo wake mwema na uaminifu wake.
4 My soul is among the lions; I lie down with ravenous beasts— with men whose teeth are spears and arrows, whose tongues are sharp swords.
Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
5 Be exalted, O God, above the heavens; may Your glory cover all the earth.
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
6 They spread a net for my feet; my soul was despondent. They dug a pit before me, but they themselves have fallen into it!
Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! (Selah)
7 My heart is steadfast, O God, my heart is steadfast. I will sing and make music.
Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
8 Awake, my glory! Awake, O harp and lyre! I will awaken the dawn.
Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
9 I will praise You, O Lord, among the nations; I will sing Your praises among the peoples.
Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
10 For Your loving devotion reaches to the heavens, and Your faithfulness to the clouds.
Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
11 Be exalted, O God, above the heavens; may Your glory cover all the earth.
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.

< Psalms 57 >