< Psalms 48 >
1 A song. A Psalm of the sons of Korah. Great is the LORD, and greatly to be praised in the city of our God, His holy mountain.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Beautiful in loftiness, the joy of all the earth, like the peaks of Zaphon is Mount Zion, the city of the great King.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 God is in her citadels; He has shown Himself to be a fortress.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 For behold, the kings assembled; they all advanced together.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 They saw and were astounded; they fled in terror.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Trembling seized them there, anguish like a woman in labor.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 With a wind from the east You wrecked the ships of Tarshish.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 As we have heard, so we have seen in the city of the LORD of Hosts, in the city of our God: God will establish her forever.
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 Within Your temple, O God, we contemplate Your loving devotion.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 Your name, O God, like Your praise, reaches to the ends of the earth; Your right hand is full of righteousness.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Mount Zion is glad, the daughters of Judah rejoice, on account of Your judgments.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 March around Zion, encircle her, count her towers,
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 consider her ramparts, tour her citadels, that you may tell the next generation.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 For this God is our God forever and ever; He will be our guide even till death.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.