< Psalms 45 >

1 For the choirmaster. To the tune of “The Lilies.” A Maskil of the sons of Korah. A love song. My heart is stirred by a noble theme as I recite my verses to the king; my tongue is the pen of a skillful writer.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 You are the most handsome of men; grace has anointed your lips, since God has blessed you forever.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Strap your sword at your side, O mighty warrior; appear in your majesty and splendor.
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 In your splendor ride forth in victory on behalf of truth and humility and justice; may your right hand show your awesome deeds.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Your arrows pierce the hearts of the king’s foes; the nations fall beneath your feet.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 Your throne, O God, endures forever and ever, and justice is the scepter of Your kingdom.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 You have loved righteousness and hated wickedness; therefore God, your God, has anointed you above your companions with the oil of joy.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 All your garments are fragrant with myrrh and aloes and cassia; from palaces of ivory the harps make you glad.
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 The daughters of kings are among your honored women; the queen stands at your right hand, adorned with the gold of Ophir.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Listen, O daughter! Consider and incline your ear: Forget your people and your father’s house,
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 and the king will desire your beauty; bow to him, for he is your lord.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 The Daughter of Tyre will come with a gift; men of wealth will seek your favor.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 All glorious is the princess in her chamber; her gown is embroidered with gold.
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 In colorful garments she is led to the king; her virgin companions are brought before you.
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 They are led in with joy and gladness; they enter the palace of the king.
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 Your sons will succeed your fathers; you will make them princes throughout the land.
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 I will commemorate your name through all generations; therefore the nations will praise you forever and ever.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

< Psalms 45 >