< Psalms 4 >
1 For the choirmaster. With stringed instruments. A Psalm of David. Answer me when I call, O God of my righteousness! You have relieved my distress; show me grace and hear my prayer.
Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
2 How long, O men, will my honor be maligned? How long will you love vanity and seek after lies?
Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
3 Know that the LORD has set apart the godly for Himself; the LORD hears when I call to Him.
Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
4 Be angry, yet do not sin; on your bed, search your heart and be still.
Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
5 Offer the sacrifices of the righteous and trust in the LORD.
Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
6 Many ask, “Who can show us the good?” Shine the light of Your face upon us, O LORD.
Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
7 You have filled my heart with more joy than when grain and new wine abound.
Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
8 I will lie down and sleep in peace, for You alone, O LORD, make me dwell in safety.
Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.