< Psalms 34 >

1 Of David, when he pretended to be insane before Abimelech, so that the king drove him away. I will bless the LORD at all times; His praise will always be on my lips.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 My soul boasts in the LORD; let the oppressed hear and rejoice.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Magnify the LORD with me; let us exalt His name together.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 I sought the LORD, and He answered me; He delivered me from all my fears.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Those who look to Him are radiant with joy; their faces shall never be ashamed.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 This poor man called out, and the LORD heard him; He saved him from all his troubles.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 The angel of the LORD encamps around those who fear Him, and he delivers them.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Taste and see that the LORD is good; blessed is the man who takes refuge in Him!
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Fear the LORD, you His saints, for those who fear Him lack nothing.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Young lions go lacking and hungry, but those who seek the LORD lack no good thing.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Come, children, listen to me; I will teach you the fear of the LORD.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Who is the man who delights in life, who desires to see good days?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Keep your tongue from evil and your lips from deceitful speech.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Turn away from evil and do good; seek peace and pursue it.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 The eyes of the LORD are on the righteous, and His ears are inclined to their cry.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 But the face of the LORD is against those who do evil, to wipe out all memory of them from the earth.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 The righteous cry out, and the LORD hears; He delivers them from all their troubles.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 The LORD is near to the brokenhearted; He saves the contrite in spirit.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Many are the afflictions of the righteous, but the LORD delivers him from them all.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 He protects all his bones; not one of them will be broken.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Evil will slay the wicked, and the haters of the righteous will be condemned.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 The LORD redeems His servants, and none who take refuge in Him will be condemned.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalms 34 >