< Psalms 3 >
1 A Psalm of David, when he fled from his son Absalom. O LORD, how my foes have increased! How many rise up against me!
Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2 Many say of me, “God will not deliver him.”
Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
3 But You, O LORD, are a shield around me, my glory, and the One who lifts my head.
Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4 To the LORD I cry aloud, and He answers me from His holy mountain.
Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5 I lie down and sleep; I wake again, for the LORD sustains me.
Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
6 I will not fear the myriads set against me on every side.
Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7 Arise, O LORD! Save me, O my God! Strike all my enemies on the jaw; break the teeth of the wicked.
Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
8 Salvation belongs to the LORD; may Your blessing be on Your people.
Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.