< Psalms 142 >
1 A Maskil of David, when he was in the cave. A prayer. I cry aloud to the LORD; I lift my voice to the LORD for mercy.
Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
2 I pour out my complaint before Him; I reveal my trouble to Him.
Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
3 Although my spirit grows faint within me, You know my way. Along the path I travel they have hidden a snare for me.
Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
4 Look to my right and see; no one attends to me. There is no refuge for me; no one cares for my soul.
Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
5 I cry to You, O LORD: “You are my refuge, my portion in the land of the living.”
Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 Listen to my cry, for I am brought quite low. Rescue me from my pursuers, for they are too strong for me.
Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Free my soul from prison, that I may praise Your name. The righteous will gather around me because of Your goodness to me.
Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”