< Psalms 142 >
1 A Maskil of David, when he was in the cave. A prayer. I cry aloud to the LORD; I lift my voice to the LORD for mercy.
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
2 I pour out my complaint before Him; I reveal my trouble to Him.
Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
3 Although my spirit grows faint within me, You know my way. Along the path I travel they have hidden a snare for me.
Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
4 Look to my right and see; no one attends to me. There is no refuge for me; no one cares for my soul.
Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
5 I cry to You, O LORD: “You are my refuge, my portion in the land of the living.”
Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 Listen to my cry, for I am brought quite low. Rescue me from my pursuers, for they are too strong for me.
Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 Free my soul from prison, that I may praise Your name. The righteous will gather around me because of Your goodness to me.
Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.