< Psalms 127 >
1 A song of ascents. Of Solomon. Unless the LORD builds the house, its builders labor in vain; unless the LORD protects the city, its watchmen stand guard in vain.
Yahwe asipoijenga nyumba, waijengao wafanya kazi bure. Yahwe asipoulinda mji, aulindaye afanya kazi bure.
2 In vain you rise early and stay up late, toiling for bread to eat— for He gives sleep to His beloved.
Ni kazi bure kwa wewe unayeamka mapema, na kulala kwa kuchelewa, au kula mkate kwa kuufanyia kazi ngumu, maana Yahwe huwapa chakula awapendao hata wawapo usingizini.
3 Children are indeed a heritage from the LORD, and the fruit of the womb is His reward.
Tazama, wana ni urithi kutoka kwa Yahwe, uzao wa tumbo ni thawabu kutoka kwake.
4 Like arrows in the hand of a warrior, so are children born in one’s youth.
Kama mishale mkononi mwa shujaa, ndivyo walivyo wana wa ujanani.
5 Blessed is the man whose quiver is full of them. He will not be put to shame when he confronts the enemies at the gate.
Ni namna gani alivyo barikiwa mtu ambaye amelijaza podo lake hivyo. Hata aibishwa pindi atakapo kabiliana na adui zake katika lango.