< Psalms 125 >
1 A song of ascents. Those who trust in the LORD are like Mount Zion. It cannot be moved; it abides forever.
Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
2 As the mountains surround Jerusalem, so the LORD surrounds His people, both now and forevermore.
Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
3 For the scepter of the wicked will not rest upon the land allotted to the righteous, so that the righteous will not put forth their hands to injustice.
Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi waliopewa wenye haki, ili wenye haki wasije wakatumia mikono yao kutenda ubaya.
4 Do good, O LORD, to those who are good, and to the upright in heart.
Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
5 But those who turn to crooked ways the LORD will banish with the evildoers. Peace be upon Israel.
Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.