< Psalms 111 >
1 Hallelujah! I will give thanks to the LORD with all my heart in the council of the upright and in the assembly.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 Great are the works of the LORD; they are pondered by all who delight in them.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 Splendid and majestic is His work; His righteousness endures forever.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 He has caused His wonders to be remembered; the LORD is gracious and compassionate.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 He provides food for those who fear Him; He remembers His covenant forever.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 He has shown His people the power of His works by giving them the inheritance of the nations.
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 The works of His hands are truth and justice; all His precepts are trustworthy.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 They are upheld forever and ever, enacted in truth and uprightness.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 He has sent redemption to His people; He has ordained His covenant forever; holy and awesome is His name.
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 The fear of the LORD is the beginning of wisdom; all who follow His precepts gain rich understanding. His praise endures forever!
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.