< Psalms 106 >

1 Hallelujah! Give thanks to the LORD, for He is good; His loving devotion endures forever.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Who can describe the mighty acts of the LORD or fully proclaim His praise?
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Blessed are those who uphold justice, who practice righteousness at all times.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Remember me, O LORD, in Your favor to Your people; visit me with Your salvation,
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 that I may see the prosperity of Your chosen ones, and rejoice in the gladness of Your nation, and give glory with Your inheritance.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 We have sinned like our fathers; we have done wrong and acted wickedly.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Our fathers in Egypt did not grasp Your wonders or remember Your abundant kindness; but they rebelled by the sea, there at the Red Sea.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Yet He saved them for the sake of His name, to make His power known.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 He rebuked the Red Sea, and it dried up; He led them through the depths as through a desert.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 He saved them from the hand that hated them; He redeemed them from the hand of the enemy.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 The waters covered their foes; not one of them remained.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Then they believed His promises and sang His praise.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 Yet they soon forgot His works and failed to wait for His counsel.
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 They craved intensely in the wilderness and tested God in the desert.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 So He granted their request, but sent a wasting disease upon them.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 In the camp they envied Moses, as well as Aaron, the holy one of the LORD.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 The earth opened up and swallowed Dathan; it covered the assembly of Abiram.
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 Then fire blazed through their company; flames consumed the wicked.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 At Horeb they made a calf and worshiped a molten image.
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 They exchanged their Glory for the image of a grass-eating ox.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 They forgot God their Savior, who did great things in Egypt,
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 wondrous works in the land of Ham, and awesome deeds by the Red Sea.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 So He said He would destroy them— had not Moses His chosen one stood before Him in the breach to divert His wrath from destroying them.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 They despised the pleasant land; they did not believe His promise.
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 They grumbled in their tents and did not listen to the voice of the LORD.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 So He raised His hand and swore to cast them down in the wilderness,
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 to disperse their offspring among the nations and scatter them throughout the lands.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 They yoked themselves to Baal of Peor and ate sacrifices offered to lifeless gods.
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 So they provoked the LORD to anger with their deeds, and a plague broke out among them.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 But Phinehas stood and intervened, and the plague was restrained.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 It was credited to him as righteousness for endless generations to come.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 At the waters of Meribah they angered the LORD, and trouble came to Moses because of them.
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 For they rebelled against His Spirit, and Moses spoke rashly with his lips.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 They did not destroy the peoples as the LORD had commanded them,
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 but they mingled with the nations and adopted their customs.
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 They worshiped their idols, which became a snare to them.
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 They sacrificed their sons and their daughters to demons.
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 They shed innocent blood— the blood of their sons and daughters, whom they sacrificed to the idols of Canaan, and the land was polluted with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 They defiled themselves by their actions and prostituted themselves by their deeds.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 So the anger of the LORD burned against His people, and He abhorred His own inheritance.
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 He delivered them into the hand of the nations, and those who hated them ruled over them.
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Their enemies oppressed them, and subdued them under their hand.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Many times He rescued them, but they were bent on rebellion and sank down in their iniquity.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 Nevertheless He heard their cry; He took note of their distress.
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 And He remembered His covenant with them, and relented by the abundance of His loving devotion.
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 He made them objects of compassion to all who held them captive.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Save us, O LORD our God, and gather us from the nations, that we may give thanks to Your holy name, that we may glory in Your praise.
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting to everlasting. Let all the people say, “Amen!” Hallelujah!
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Psalms 106 >