< Proverbs 7 >

1 My son, keep my words and treasure my commandments within you.
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Keep my commandments and live; guard my teachings as the apple of your eye.
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Tie them to your fingers; write them on the tablet of your heart.
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Say to wisdom, “You are my sister,” and call understanding your kinsman,
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 that they may keep you from the adulteress, from the stranger with seductive words.
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 For at the window of my house I looked through the lattice.
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 I saw among the simple, I noticed among the youths, a young man lacking judgment,
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 crossing the street near her corner, strolling down the road to her house,
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 at twilight, as the day was fading into the dark of the night.
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 Then a woman came out to meet him, with the attire of a harlot and cunning of heart.
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 She is loud and defiant; her feet do not remain at home.
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 Now in the street, now in the squares, she lurks at every corner.
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 She seizes him and kisses him; she brazenly says to him:
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 “I have made my peace offerings; today I have paid my vows.
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 So I came out to meet you; I sought you, and I have found you.
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 I have decked my bed with coverings, with colored linen from Egypt.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 I have perfumed my bed with myrrh, with aloes, and with cinnamon.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Come, let us take our fill of love till morning. Let us delight in loving caresses!
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 For my husband is not at home; he has gone on a long journey.
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 He took with him a bag of money and will not return till the moon is full.”
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 With her great persuasion she entices him; with her flattering lips she lures him.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 He follows her on impulse, like an ox going to the slaughter, like a deer bounding into a trap,
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 until an arrow pierces his liver, like a bird darting into a snare— not knowing it will cost him his life.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 Now, my sons, listen to me, and attend to the words of my mouth.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 Do not let your heart turn aside to her ways; do not stray into her paths.
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 For she has brought many down to death; her slain are many in number.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 Her house is the road to Sheol, descending to the chambers of death. (Sheol h7585)
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< Proverbs 7 >