< Matthew 25 >
1 “At that time the kingdom of heaven will be like ten virgins who took their lamps and went out to meet the bridegroom.
“Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2 Five of them were foolish, and five were wise.
Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3 The foolish ones took their lamps but did not take along any extra oil.
Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4 But the wise ones took oil in flasks along with their lamps.
Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5 When the bridegroom was delayed, they all became drowsy and fell asleep.
Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6 At midnight the cry rang out: ‘Here is the bridegroom! Come out to meet him!’
Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7 Then all the virgins woke up and trimmed their lamps.
Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8 The foolish ones said to the wise, ‘Give us some of your oil; our lamps are going out.’
Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9 ‘No,’ said the wise ones, ‘or there may not be enough for both us and you. Instead, go to those who sell oil and buy some for yourselves.’
Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10 But while they were on their way to buy it, the bridegroom arrived. Those who were ready went in with him to the wedding banquet, and the door was shut.
Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11 Later the other virgins arrived and said, ‘Lord, lord, open the door for us!’
Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12 But he replied, ‘Truly I tell you, I do not know you.’
Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi.”
13 Therefore keep watch, because you do not know the day or the hour.
Kisha Yesu akasema, “Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14 For it is just like a man going on a journey, who called his servants and entrusted them with his possessions.
“Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15 To one he gave five talents, to another two talents, and to another one talent—each according to his own ability. And he went on his journey.
Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16 The servant who had received the five talents went at once and put them to work and gained five more.
Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17 Likewise, the one with the two talents gained two more.
Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18 But the servant who had received the one talent went off, dug a hole in the ground, and hid his master’s money.
Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19 After a long time the master of those servants returned to settle accounts with them.
“Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20 The servant who had received the five talents came and presented five more. ‘Master,’ he said, ‘you entrusted me with five talents. See, I have gained five more.’
Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21 His master replied, ‘Well done, good and faithful servant! You have been faithful with a few things; I will put you in charge of many things. Enter into the joy of your master!’
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22 The servant who had received the two talents also came and said, ‘Master, you entrusted me with two talents. See, I have gained two more.’
“Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23 His master replied, ‘Well done, good and faithful servant! You have been faithful with a few things; I will put you in charge of many things. Enter into the joy of your master!’
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24 Finally, the servant who had received the one talent came and said, ‘Master, I knew that you are a hard man, reaping where you have not sown and gathering where you have not scattered seed.
“Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25 So I was afraid and went out and hid your talent in the ground. See, you have what belongs to you.’
Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26 ‘You wicked, lazy servant!’ replied his master. ‘You knew that I reap where I have not sown and gather where I have not scattered seed.
“Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27 Then you should have deposited my money with the bankers, and on my return I would have received it back with interest.
Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28 Therefore take the talent from him and give it to the one who has ten talents.
Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29 For everyone who has will be given more, and he will have an abundance. But the one who does not have, even what he has will be taken away from him.
Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30 And throw that worthless servant into the outer darkness, where there will be weeping and gnashing of teeth.’
Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31 When the Son of Man comes in His glory, and all the angels with Him, He will sit on His glorious throne.
“Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32 All the nations will be gathered before Him, and He will separate the people one from another, as a shepherd separates the sheep from the goats.
na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33 He will place the sheep on His right and the goats on His left.
Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34 Then the King will say to those on His right, ‘Come, you who are blessed by My Father, inherit the kingdom prepared for you from the foundation of the world.
“Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35 For I was hungry and you gave Me something to eat, I was thirsty and you gave Me something to drink, I was a stranger and you took Me in,
Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36 I was naked and you clothed Me, I was sick and you looked after Me, I was in prison and you visited Me.’
nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37 Then the righteous will answer Him, ‘Lord, when did we see You hungry and feed You, or thirsty and give You something to drink?
Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38 When did we see You a stranger and take You in, or naked and clothe You?
Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39 When did we see You sick or in prison and visit You?’
Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40 And the King will reply, ‘Truly I tell you, whatever you did for one of the least of these brothers of Mine, you did for Me.’
Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41 Then He will say to those on His left, ‘Depart from Me, you who are cursed, into the eternal fire prepared for the devil and his angels. (aiōnios )
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake. (aiōnios )
42 For I was hungry and you gave Me nothing to eat, I was thirsty and you gave Me nothing to drink,
Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43 I was a stranger and you did not take Me in, I was naked and you did not clothe Me, I was sick and in prison and you did not visit Me.’
Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44 And they too will reply, ‘Lord, when did we see You hungry or thirsty or a stranger or naked or sick or in prison, and did not minister to You?’
“Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45 Then the King will answer, ‘Truly I tell you, whatever you did not do for one of the least of these, you did not do for Me.’
Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46 And they will go away into eternal punishment, but the righteous into eternal life.” (aiōnios )
Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele.” (aiōnios )