< Mark 3 >
1 Once again Jesus entered the synagogue, and a man with a withered hand was there.
Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
2 In order to accuse Jesus, they were watching to see if He would heal on the Sabbath.
Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
3 Then Jesus said to the man with the withered hand, “Stand up among us.”
Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
4 And He asked them, “Which is lawful on the Sabbath: to do good or to do evil, to save life or to destroy it?” But they were silent.
Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
5 Jesus looked around at them with anger and sorrow at their hardness of heart. Then He said to the man, “Stretch out your hand.” So he stretched it out, and it was restored.
Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
6 At this, the Pharisees went out and began plotting with the Herodians how they might kill Jesus.
Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
7 So Jesus withdrew with His disciples to the sea, accompanied by a large crowd from Galilee, Judea,
Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
8 Jerusalem, Idumea, the region beyond the Jordan, and the vicinity of Tyre and Sidon. The large crowd came to Him when they heard what great things He was doing.
Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
9 Jesus asked His disciples to have a boat ready for Him so that the crowd would not crush Him.
Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
10 For He had healed so many that all who had diseases were pressing forward to touch Him.
Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
11 And when the unclean spirits saw Him, they fell down before Him and cried out, “You are the Son of God!”
Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
12 But He warned them sternly not to make Him known.
Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
13 Then Jesus went up on the mountain and called for those He wanted, and they came to Him.
Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
14 He appointed twelve of them, whom He designated as apostles, to accompany Him, to be sent out to preach,
Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
15 and to have authority to drive out demons.
na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
16 These are the twelve He appointed: Simon (whom He named Peter),
Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
17 James son of Zebedee and his brother John (whom He named Boanerges, meaning “Sons of Thunder”),
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
18 Andrew, Philip, Bartholomew, Matthew, Thomas, James son of Alphaeus, Thaddaeus, Simon the Zealot,
Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 and Judas Iscariot, who betrayed Jesus.
na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
20 Then Jesus went home, and once again a crowd gathered, so that He and His disciples could not even eat.
Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
21 When His family heard about this, they went out to take custody of Him, saying, “He is out of His mind.”
Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
22 And the scribes who had come down from Jerusalem were saying, “He is possessed by Beelzebul,” and, “By the prince of the demons He drives out demons.”
Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
23 So Jesus called them together and began to speak to them in parables: “How can Satan drive out Satan?
Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
24 If a kingdom is divided against itself, it cannot stand.
Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 If a house is divided against itself, it cannot stand.
Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 And if Satan is divided and rises against himself, he cannot stand; his end has come.
Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
27 Indeed, no one can enter a strong man’s house to steal his possessions unless he first ties up the strong man. Then he can plunder his house.
Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
28 Truly I tell you, the sons of men will be forgiven all sins and blasphemies, as many as they utter.
Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
29 But whoever blasphemes against the Holy Spirit will never be forgiven; he is guilty of eternal sin.” (aiōn , aiōnios )
Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn , aiōnios )
30 Jesus made this statement because they were saying, “He has an unclean spirit.”
Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
31 Then Jesus’ mother and brothers came and stood outside. They sent someone in to summon Him,
Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
32 and a crowd was sitting around Him. “Look,” He was told, “Your mother and brothers are outside, asking for You.”
Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
33 But Jesus replied, “Who are My mother and My brothers?”
Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
34 Looking at those seated in a circle around Him, He said, “Here are My mother and My brothers!
Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 For whoever does the will of God is My brother and sister and mother.”
Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”