< Mark 15 >
1 Early in the morning, the chief priests, elders, scribes, and the whole Sanhedrin devised a plan. They bound Jesus, led Him away, and handed Him over to Pilate.
Asubuhi na mapema wakuu wa makuhani walikutana pamoja na wazee na waandishi na baraza zima la wazee. Kisha wakamfunga Yesu wakampeleka kwa Pilato. Pilato akamwuliza, “wewe ni Mfalme wa Wayahudi?”
2 So Pilate questioned Him, “Are You the King of the Jews?” “You have said so,” Jesus replied.
“Akamjibu, “Wewe umesema hivyo.”
3 And the chief priests began to accuse Him of many things.
Wakuu wa makuhani wakaeleza mashitaka mengi juu ya Yesu.
4 Then Pilate questioned Him again, “Have You no answer? Look how many charges they are bringing against You!”
Pilato akamwuliza tena, “Hujibu chochote? Huoni jinsi wanavyokushtaki kwa mambo mengi?
5 But to Pilate’s amazement, Jesus made no further reply.
Lakini Yesu hakumjibu Pilato, na hiyo ilimshangaza.
6 Now it was Pilate’s custom at the feast to release to the people a prisoner of their choosing.
Kwa kawaida wakati wa sikukuu humfungulia mfungwa mmoja, mfungwa waliyemwomba.
7 And a man named Barabbas was imprisoned with the rebels who had committed murder during the insurrection.
Kulikuwapo wahalifu gerezani, miongoni mwa wauaji kati ya walioasi wanaotumikia makosa yao. Alikuwepo mtu mmoja aitwaye Baraba.
8 So the crowd went up and began asking Pilate to keep his custom.
Umati ulikuja kwa Pilato, na kumwomba afanye kama alivyofanya huko nyuma.
9 “Do you want me to release to you the King of the Jews?” Pilate asked.
Pilato akawajibu na kusema, “Mnataka niwafungulie Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he knew it was out of envy that the chief priests had handed Jesus over.
Kwa kuwa alijua ni kwa sababu ya wivu wakuu wa makuhani walimkamata Yesu na kumleta kwake.
11 But the chief priests stirred up the crowd to have him release Barabbas to them instead.
Lakini wakuu wa makuhani walichochea umati kupiga kelele kwa sauti kwamba afunguliwe Baraba badala yake.
12 So Pilate asked them again, “What then do you want me to do with the One you call the King of the Jews?”
Pilato akawajibu tena na kusema, “Nimfanye nini Mfalme wa Wayahudi?
13 And they shouted back, “Crucify Him!”
Wakapiga kelele tena, “Msulibishe!”
14 “Why?” asked Pilate. “What evil has He done?” But they shouted all the louder, “Crucify Him!”
Pilato akasema, “Amefanya jambo gani baya?” Lakini wakazidi kupiga kelele zaidi na zaidi “Msulibishe.”
15 And wishing to satisfy the crowd, Pilate released Barabbas to them. But he had Jesus flogged, and handed Him over to be crucified.
Pilato akitaka kuwaridhisha umati, akawafungulia Baraba. Akampiga Yesu mijeledi kisha akamtoa ili asulibiwe.
16 Then the soldiers led Jesus away into the palace (that is, the Praetorium) and called the whole company together.
Askari walimwongoza hadi ndani ya ua (ule ulio ndani ya kambi) na walikusanyika pamoja kikosi cha askari.
17 They dressed Him in a purple robe, twisted together a crown of thorns, and set it on His head.
Wakamvika Yesu kanzu ya rangi ya zambarau, na wakasokota taji ya miiba wakamvika.
18 And they began to salute Him: “Hail, King of the Jews!”
Wakaanza kumdhihaki na kusema, “Salam, Mfalme wa Wayahudi!”
19 They kept striking His head with a staff and spitting on Him. And they knelt down and bowed before Him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake kwa kumheshimu.
20 After they had mocked Him, they removed the purple robe and put His own clothes back on Him. Then they led Him out to crucify Him.
Hata wakiisha kumdhihaki, wakamvua ile kanzu ya rangi ya zambarau na kumvika mavazi yake, na wakamtoa nje kwenda kumsulibisha.
21 Now Simon of Cyrene, the father of Alexander and Rufus, was passing by on his way in from the country, and the soldiers forced him to carry the cross of Jesus.
Wakamlazimisha mpita njia kumsaidia, aliyekuwa anaingia mjini kutoka shamba. Aitwaye Simoni Mkirene (baba yake Iskanda na Rufo); wakamlazimisha kubeba msalaba wa Yesu.
22 They brought Jesus to a place called Golgotha, which means The Place of the Skull.
Askari wakampeleka Yesu mahali paitwapo Goligotha (maana ya tafsiri hii ni, Sehemu ya Fuvu la kichwa).
23 There they offered Him wine mixed with myrrh, but He did not take it.
Wakampa mvinyo iliyochanganywa na manemane, lakini hakunywa.
24 And they crucified Him. They also divided His garments by casting lots to decide what each of them would take.
Wakamsulibisha na wakagawana mavazi yake, wakayapigia kura kuamua kipande atakachopata kila askari.
25 It was the third hour when they crucified Him.
Yapata saa tatu asubuhi walipomsulibisha.
26 And the charge inscribed against Him read: THE KING OF THE JEWS.
Wakaweka juu yake ubao ulioandikwa shitaka, “Mfalme wa Wayahudi.”
27 Along with Jesus, they crucified two robbers, one on His right and one on His left.
Walimsubisha pamoja na majambazi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine kushoto kwake.
(Zingatia: Mstari huu, “Na maandiko yakatimia yaliyonena” haumo katika nakala za kale).
29 And those who passed by heaped abuse on Him, shaking their heads and saying, “Aha! You who are going to destroy the temple and rebuild it in three days,
Nao waliokuwa wakipita walimtukana, wakitikisa vichwa vyao wakisema, “Aha! wewe utakayevunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 come down from the cross and save Yourself!”
jiokoe mwenyewe na ushuke chini toka msalabani!”
31 In the same way, the chief priests and scribes mocked Him among themselves, saying, “He saved others, but He cannot save Himself!
Kwa namna ile ile wakuu wa makuhani walimdhihaki wakisemezana, pamoja na waandishi na kusema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe.
32 Let the Christ, the King of Israel, come down now from the cross, so that we may see and believe!” And even those who were crucified with Him berated Him.
Kristo Mfalme wa Israel, shuka chini sasa toka msalabani, ili tuweze kuona na kuamini.” Na wale waliosulubiwa pamoja naye pia walimdhihaki.
33 From the sixth hour until the ninth hour darkness came over all the land.
Ilipofika saa sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa tisa.
34 At the ninth hour, Jesus cried out in a loud voice, “Eloi, Eloi, lema sabachthani?” which means, “My God, My God, why have You forsaken Me?”
Wakati wa saa tisa, Yesu alipiga kelele kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lama sabaktani?” ikiwa na maana “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
35 When some of those standing nearby heard this, they said, “Behold, He is calling Elijah.”
Baadhi ya hao waliosimama waliposikia wakasema, “Tazama, anamwita Eliya.”
36 And someone ran and filled a sponge with sour wine. He put it on a reed and held it up for Jesus to drink, saying, “Leave Him alone. Let us see if Elijah comes to take Him down.”
Mtu mmoja akakimbia, akajaza siki katika sponji na kuiweka juu ya mti wa mwanzi, akampa ili anywe. Mtu mmoja akasema, “Ngoja tuone kama Eliya atakuja kumshusha chini.”
37 But Jesus let out a loud cry and breathed His last.
Kisha Yesu akalia kwa sauti kubwa na akafa.
38 And the veil of the temple was torn in two from top to bottom.
Pazia la hekalu likagawanyika vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 When the centurion standing there in front of Jesus saw how He had breathed His last, he said, “Truly this man was the Son of God!”
Ofisa mmoja aliyekuwa amesimama akimwelekea Yesu, alipoona amekufa kwa jinsi ile, akasema, “Kweli huyu mtu alikuwa Mwana wa Mungu.”
40 And there were also women watching from a distance. Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James the younger and of Joses, and Salome.
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakitazama kwa mbali. Miongoni mwao alikuwepo Mariamu Magdalena, Mariamu (mama yake Yakobo mdogo wa Yose), na Salome.
41 These women had followed Jesus and ministered to Him while He was in Galilee, and there were many other women who had come up to Jerusalem with Him.
Wakati alipokuwa Galilaya walimfuata na kumtumikia. Na wanawake wengine wengi pia waliambatana naye hadi Yerusalemu.
42 Now it was already evening. Since it was Preparation Day (that is, the day before the Sabbath),
Kulipokuwa jioni, na kwa kuwa ilikuwa siku ya maandalio, siku kabla ya Sabato,
43 Joseph of Arimathea, a prominent Council member who himself was waiting for the kingdom of God, boldly went to Pilate to ask for the body of Jesus.
Yusufu wa Arimathaya alikuja pale. Alikuwa ni mjumbe wa Baraza anayeheshimiwa mtu anayeutarajia Ufalme wa Mungu. Kwa ujasiri akaenda kwa Pilato, na kuuomba mwili wa Yesu.
44 Pilate was surprised to hear that Jesus was already dead, so he summoned the centurion to ask if this was so.
Pilato akashangazwa kwamba Yesu tayari amekufa; akamwita yule afisa akamwuliza kama Yesu amekufa.
45 When Pilate had confirmed it with the centurion, he granted the body to Joseph.
Alipopata uhakika kwa afisa kwamba amekufa, alimruhusu Yusufu kuuchukua mwili.
46 So Joseph bought a linen cloth, took down the body of Jesus, wrapped it in the cloth, and placed it in a tomb that had been cut out of the rock. Then he rolled a stone against the entrance to the tomb.
Yusufu alikuwa amenunua sanda. Akamshusha toka msalabani, akamfunga kwa sanda, na kumweka ndani ya kaburi lililochimbwa katika mwamba. Kisha akalivingirisha jiwe mlangoni mwa kaburi.
47 Mary Magdalene and Mary the mother of Joseph saw where His body was placed.
Mariamu Magdalena na Mariamu mama yake Yose waliona sehemu alipozikwa Yesu.