< John 2 >

1 On the third day a wedding took place at Cana in Galilee. Jesus’ mother was there,
Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
2 and Jesus and His disciples had also been invited to the wedding.
Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
3 When the wine ran out, Jesus’ mother said to Him, “They have no more wine.”
Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
4 “Woman, why does this concern us?” Jesus replied. “My hour has not yet come.”
Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
5 His mother said to the servants, “Do whatever He tells you.”
Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
6 Now six stone water jars had been set there for the Jewish rites of purification. Each could hold from twenty to thirty gallons.
Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
7 Jesus told the servants, “Fill the jars with water.” So they filled them to the brim.
Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
8 “Now draw some out,” He said, “and take it to the master of the banquet.” They did so,
Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
9 and the master of the banquet tasted the water that had been turned into wine. He did not know where it was from, but the servants who had drawn the water knew. Then he called the bridegroom aside
Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
10 and said, “Everyone serves the fine wine first, and then the cheap wine after the guests are drunk. But you have saved the fine wine until now!”
akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
11 Jesus performed this, the first of His signs, at Cana in Galilee. He thus revealed His glory, and His disciples believed in Him.
Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
12 After this, He went down to Capernaum with His mother and brothers and His disciples, and they stayed there a few days.
Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
13 When the Jewish Passover was near, Jesus went up to Jerusalem.
Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
14 In the temple courts He found men selling cattle, sheep, and doves, and money changers seated at their tables.
Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
15 So He made a whip out of cords and drove all from the temple courts, both sheep and cattle. He poured out the coins of the money changers and overturned their tables.
Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
16 To those selling doves He said, “Get these out of here! How dare you turn My Father’s house into a marketplace!”
Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
17 His disciples remembered that it is written: “Zeal for Your house will consume Me.”
Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
18 On account of this, the Jews demanded, “What sign can You show us to prove Your authority to do these things?”
Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
19 Jesus answered, “Destroy this temple, and in three days I will raise it up again.”
Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
20 “This temple took forty-six years to build,” the Jews replied, “and You are going to raise it up in three days?”
Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
21 But Jesus was speaking about the temple of His body.
Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
22 After He was raised from the dead, His disciples remembered that He had said this. Then they believed the Scripture and the word that Jesus had spoken.
Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
23 While He was in Jerusalem at the Passover Feast, many people saw the signs He was doing and believed in His name.
Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
24 But Jesus did not entrust Himself to them, for He knew them all.
Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
25 He did not need any testimony about man, for He knew what was in a man.
Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.

< John 2 >