< John 17 >

1 When Jesus had spoken these things, He lifted up His eyes to heaven and said, “Father, the hour has come. Glorify Your Son, that Your Son may glorify You.
Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
2 For You granted Him authority over all people, so that He may give eternal life to all those You have given Him. (aiōnios g166)
Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios g166)
3 Now this is eternal life, that they may know You, the only true God, and Jesus Christ, whom You have sent. (aiōnios g166)
Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
4 I have glorified You on earth by accomplishing the work You gave Me to do.
Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
5 And now, Father, glorify Me in Your presence with the glory I had with You before the world existed.
Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
6 I have revealed Your name to those You have given Me out of the world. They were Yours; You gave them to Me, and they have kept Your word.
“Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
7 Now they know that everything You have given Me comes from You.
Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
8 For I have given them the words You gave Me, and they have received them. They knew with certainty that I came from You, and they believed that You sent Me.
kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
9 I ask on their behalf. I do not ask on behalf of the world, but on behalf of those You have given Me; for they are Yours.
Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
10 All I have is Yours, and all You have is Mine; and in them I have been glorified.
Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
11 I will no longer be in the world, but they are in the world, and I am coming to You. Holy Father, protect them by Your name, the name You gave Me, so that they may be one as We are one.
Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
12 While I was with them, I protected and preserved them by Your name, the name You gave Me. Not one of them has been lost, except the son of destruction, so that the Scripture would be fulfilled.
Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
13 But now I am coming to You; and I am saying these things while I am in the world, so that they may have My joy fulfilled within them.
“Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
14 I have given them Your word and the world has hated them; for they are not of the world, just as I am not of the world.
Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
15 I am not asking that You take them out of the world, but that You keep them from the evil one.
Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
16 They are not of the world, just as I am not of the world.
Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
17 Sanctify them by the truth; Your word is truth.
Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
18 As You sent Me into the world, I have also sent them into the world.
Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
19 For them I sanctify Myself, so that they too may be sanctified by the truth.
Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
20 I am not asking on behalf of them alone, but also on behalf of those who will believe in Me through their message,
“Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
21 that all of them may be one, as You, Father, are in Me, and I am in You. May they also be in Us, so that the world may believe that You sent Me.
ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
22 I have given them the glory You gave Me, so that they may be one as We are one—
Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
23 I in them and You in Me—that they may be perfectly united, so that the world may know that You sent Me and have loved them just as You have loved Me.
Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
24 Father, I want those You have given Me to be with Me where I am, that they may see the glory You gave Me because You loved Me before the foundation of the world.
“Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
25 Righteous Father, although the world has not known You, I know You, and they know that You sent Me.
“Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
26 And I have made Your name known to them and will continue to make it known, so that the love You have for Me may be in them, and I in them.”
Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”

< John 17 >