< Job 9 >
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 “Yes, I know that it is so, but how can a mortal be righteous before God?
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 If one wished to contend with God, he could not answer Him one time out of a thousand.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 God is wise in heart and mighty in strength. Who has resisted Him and prospered?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 He moves mountains without their knowledge and overturns them in His anger.
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 He shakes the earth from its place, so that its foundations tremble.
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 He commands the sun not to shine; He seals off the stars.
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 He alone stretches out the heavens and treads on the waves of the sea.
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 He is the Maker of the Bear and Orion, of the Pleiades and the constellations of the south.
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 He does great things beyond searching out, and wonders without number.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Were He to pass by me, I would not see Him; were He to move, I would not recognize Him.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 If He takes away, who can stop Him? Who dares to ask Him, ‘What are You doing?’
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 God does not restrain His anger; the helpers of Rahab cower beneath Him.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 How then can I answer Him or choose my arguments against Him?
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 For even if I were right, I could not answer. I could only beg my Judge for mercy.
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 If I summoned Him and He answered me, I do not believe He would listen to my voice.
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 For He would crush me with a tempest and multiply my wounds without cause.
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 He does not let me catch my breath, but overwhelms me with bitterness.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 If it is a matter of strength, He is indeed mighty! If it is a matter of justice, who can summon Him?
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 Even if I were righteous, my mouth would condemn me; if I were blameless, it would declare me guilty.
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 Though I am blameless, I have no concern for myself; I despise my own life.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 It is all the same, and so I say, ‘He destroys both the blameless and the wicked.’
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 When the scourge brings sudden death, He mocks the despair of the innocent.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 The earth is given into the hand of the wicked; He blindfolds its judges. If it is not He, then who is it?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 My days are swifter than a runner; they flee without seeing good.
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 They sweep by like boats of papyrus, like an eagle swooping down on its prey.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 If I were to say, ‘I will forget my complaint and change my expression and smile,’
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 I would still dread all my sufferings; I know that You will not acquit me.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Since I am already found guilty, why should I labor in vain?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 If I should wash myself with snow and cleanse my hands with lye,
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 then You would plunge me into the pit, and even my own clothes would despise me.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 For He is not a man like me, that I can answer Him, that we can take each other to court.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 Nor is there a mediator between us, to lay his hand upon us both.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Let Him remove His rod from me, so that His terror will no longer frighten me.
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 Then I would speak without fear of Him. But as it is, I am on my own.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.