< Job 8 >
1 Then Bildad the Shuhite replied:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 “How long will you go on saying such things? The words of your mouth are a blustering wind.
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Does God pervert justice? Does the Almighty pervert what is right?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 When your children sinned against Him, He gave them over to their rebellion.
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 But if you would earnestly seek God and ask the Almighty for mercy,
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 if you are pure and upright, even now He will rouse Himself on your behalf and restore your righteous estate.
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 Though your beginnings were modest, your latter days will flourish.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Please inquire of past generations and consider the discoveries of their fathers.
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 For we were born yesterday and know nothing; our days on earth are but a shadow.
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Will they not teach you and tell you, and speak from their understanding?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Does papyrus grow where there is no marsh? Do reeds flourish without water?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 While the shoots are still uncut, they dry up quicker than grass.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Such is the destiny of all who forget God; so the hope of the godless will perish.
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 His confidence is fragile; his security is in a spider’s web.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 He leans on his web, but it gives way; he holds fast, but it does not endure.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 He is a well-watered plant in the sunshine, spreading its shoots over the garden.
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 His roots wrap around the rock heap; he looks for a home among the stones.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 If he is uprooted from his place, it will disown him, saying, ‘I never saw you.’
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Surely this is the joy of his way; yet others will spring from the dust.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Behold, God does not reject the blameless, nor will He strengthen the hand of evildoers.
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 He will yet fill your mouth with laughter, and your lips with a shout of joy.
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Your enemies will be clothed in shame, and the tent of the wicked will be no more.”
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.