< Job 37 >

1 “At this my heart also pounds and leaps from its place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Listen closely to the thunder of His voice and the rumbling that comes from His mouth.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He unleashes His lightning beneath the whole sky and sends it to the ends of the earth.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Then there comes a roaring sound; He thunders with His majestic voice. He does not restrain the lightning when His voice resounds.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God thunders wondrously with His voice; He does great things we cannot comprehend.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For He says to the snow, ‘Fall on the earth,’ and to the gentle rain, ‘Pour out a mighty downpour.’
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 He seals up the hand of every man, so that all men may know His work.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 The wild animals enter their lairs; they settle down in their dens.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 The tempest comes from its chamber, and the cold from the driving north winds.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 By the breath of God the ice is formed and the watery expanses are frozen.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 He loads the clouds with moisture; He scatters His lightning through them.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 They swirl about, whirling at His direction, accomplishing all that He commands over the face of all the earth.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Whether for punishment or for His land, He accomplishes this in His loving devotion.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Listen to this, O Job; stand still and consider the wonders of God.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Do you know how God dispatches the clouds or makes the lightning flash?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Do you understand how the clouds float, those wonders of Him who is perfect in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 You whose clothes get hot when the land lies hushed under the south wind,
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 can you, like Him, spread out the skies to reflect the heat like a mirror of bronze?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Teach us what we should say to Him; we cannot draw up our case when our faces are in darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Should He be told that I want to speak? Would a man ask to be swallowed up?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Now no one can gaze at the sun when it is bright in the skies after the wind has swept them clean.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Out of the north He comes in golden splendor; awesome majesty surrounds Him.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 The Almighty is beyond our reach; He is exalted in power! In His justice and great righteousness He does not oppress.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Therefore, men fear Him, for He is not partial to the wise in heart.”
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >