< Job 34 >
Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
2 “Hear my words, O wise men; give ear to me, O men of learning.
“Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
3 For the ear tests words as the mouth tastes food.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
4 Let us choose for ourselves what is right; let us learn together what is good.
Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
5 For Job has declared, ‘I am righteous, yet God has deprived me of justice.
Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
6 Would I lie about my case? My wound is incurable, though I am without transgression.’
Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
7 What man is like Job, who drinks up derision like water?
Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
8 He keeps company with evildoers and walks with wicked men.
ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
9 For he has said, ‘It profits a man nothing that he should delight in God.’
Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
10 Therefore listen to me, O men of understanding. Far be it from God to do wrong, and from the Almighty to act unjustly.
Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
11 For according to a man’s deeds He repays him; according to a man’s ways He brings consequences.
na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
12 Indeed, it is true that God does not act wickedly, and the Almighty does not pervert justice.
Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
13 Who gave Him charge over the earth? Who appointed Him over the whole world?
Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
14 If He were to set His heart to it and withdraw His Spirit and breath,
Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
15 all flesh would perish together and mankind would return to the dust.
basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
16 If you have understanding, hear this; listen to my words.
Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
17 Could one who hates justice govern? Will you condemn the just and mighty One,
Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
18 who says to kings, ‘You are worthless!’ and to nobles, ‘You are wicked,’
Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
19 who is not partial to princes and does not favor rich over poor? For they are all the work of His hands.
Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
20 They die in an instant, in the middle of the night. The people convulse and pass away; the mighty are removed without human hand.
Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
21 For His eyes are on the ways of a man, and He sees his every step.
Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
22 There is no darkness or deep shadow where the workers of iniquity can hide.
Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
23 For God need not examine a man further or have him approach for judgment.
Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
24 He shatters the mighty without inquiry and sets up others in their place.
Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
25 Therefore, He recognizes their deeds; He overthrows them in the night and they are crushed.
Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
26 He strikes them for their wickedness in full view,
Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
27 because they turned aside from Him and had no regard for any of His ways.
kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
28 They caused the cry of the poor to come before Him, and He heard the outcry of the afflicted.
Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
29 But when He remains silent, who can condemn Him? When He hides His face, who can see Him? Yet He watches over both man and nation,
Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 that godless men should not rule or lay snares for the people.
ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 Suppose someone says to God, ‘I have endured my punishment; I will offend no more.
Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 Teach me what I cannot see; if I have done wrong, I will not do it again.’
nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 Should God repay you on your own terms when you have disavowed His? You must choose, not I; so tell me what you know.
Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 Men of understanding will declare to me, and the wise men who hear me will say:
Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
35 ‘Job speaks without knowledge; his words lack insight.’
Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
36 If only Job were tried to the utmost for answering like a wicked man.
Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
37 For he adds rebellion to his sin; he claps his hands among us and multiplies his words against God.”
Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”