< Job 3 >

1 After this, Job opened his mouth and cursed the day of his birth.
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
2 And this is what he said:
Akasema,
3 “May the day of my birth perish, and the night it was said, ‘A boy is conceived.’
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
4 If only that day had turned to darkness! May God above disregard it; may no light shine upon it.
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
5 May darkness and gloom reclaim it, and a cloud settle over it; may the blackness of the day overwhelm it.
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
6 If only darkness had taken that night away! May it not appear among the days of the year; may it never be entered in any of the months.
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
7 Behold, may that night be barren; may no joyful voice come into it.
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
8 May it be cursed by those who curse the day — those prepared to rouse Leviathan.
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
9 May its morning stars grow dark; may it wait in vain for daylight; may it not see the breaking of dawn.
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
10 For that night did not shut the doors of the womb to hide the sorrow from my eyes.
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
11 Why did I not perish at birth; why did I not die as I came from the womb?
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
12 Why were there knees to receive me, and breasts that I should be nursed?
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
13 For now I would be lying down in peace; I would be asleep and at rest
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
14 with kings and counselors of the earth, who built for themselves cities now in ruins,
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
15 or with princes who had gold, who filled their houses with silver.
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
16 Or why was I not hidden like a stillborn child, like an infant who never sees daylight?
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
17 There the wicked cease from raging, and there the weary find rest.
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
18 The captives enjoy their ease; they do not hear the voice of the oppressor.
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
19 Both small and great are there, and the slave is freed from his master.
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
20 Why is light given to the miserable, and life to the bitter of soul,
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
21 who long for death that does not come, and search for it like hidden treasure,
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
22 who rejoice and greatly exult when they can find the grave?
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
23 Why is life given to a man whose way is hidden, whom God has hedged in?
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
24 I sigh when food is put before me, and my groans pour out like water.
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
25 For the thing I feared has overtaken me, and what I dreaded has befallen me.
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
26 I am not at ease or quiet; I have no rest, for trouble has come.”
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”

< Job 3 >