< Job 28 >
1 “Surely there is a mine for silver and a place where gold is refined.
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
2 Iron is taken from the earth, and copper is smelted from ore.
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
3 Man puts an end to the darkness; he probes the farthest recesses for ore in deepest darkness.
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
4 Far from human habitation he cuts a shaft in places forgotten by the foot of man. Far from men he dangles and sways.
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
5 Food may come from the earth, but from below it is transformed as by fire.
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
6 Its rocks are the source of sapphires, containing flecks of gold.
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
7 No bird of prey knows that path; no falcon’s eye has seen it.
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
8 Proud beasts have never trodden it; no lion has ever prowled over it.
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
9 The miner strikes the flint; he overturns mountains at their base.
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
10 He hews out channels in the rocks, and his eyes spot every treasure.
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
11 He stops up the sources of the streams to bring what is hidden to light.
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
12 But where can wisdom be found, and where does understanding dwell?
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
13 No man can know its value, nor is it found in the land of the living.
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
14 The ocean depths say, ‘It is not in me,’ while the sea declares, ‘It is not with me.’
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
15 It cannot be bought with gold, nor can its price be weighed out in silver.
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
16 It cannot be valued in the gold of Ophir, in precious onyx or sapphire.
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
17 Neither gold nor crystal can compare to it, nor jewels of fine gold be exchanged for it.
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
18 Coral and quartz are unworthy of mention; the price of wisdom is beyond rubies.
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
19 Topaz from Cush cannot compare to it, nor can it be valued in pure gold.
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
20 From where then does wisdom come, and where does understanding dwell?
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
21 It is hidden from the eyes of every living thing and concealed from the birds of the air.
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
22 Abaddon and Death say, ‘We have heard a rumor about it.’
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
23 But God understands its way, and He knows its place.
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
24 For He looks to the ends of the earth and sees everything under the heavens.
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
25 When God fixed the weight of the wind and measured out the waters,
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
26 when He set a limit for the rain and a path for the thunderbolt,
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
27 then He looked at wisdom and appraised it; He established it and searched it out.
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
28 And He said to man, ‘Behold, the fear of the Lord, that is wisdom, and to turn away from evil is understanding.’”
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”