< Job 23 >
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 “Even today my complaint is bitter. His hand is heavy despite my groaning.
“Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
3 If only I knew where to find Him, so that I could go to His seat.
Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
4 I would plead my case before Him and fill my mouth with arguments.
Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
5 I would learn how He would answer, and consider what He would say.
Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
6 Would He contend with me in His great power? No, He would certainly take note of me.
Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
7 Then an upright man could reason with Him, and I would be delivered forever from my Judge.
Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
8 If I go east, He is not there, and if I go west, I cannot find Him.
Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
9 When He is at work in the north, I cannot behold Him; when He turns to the south, I cannot see Him.
Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
10 Yet He knows the way I have taken; when He has tested me, I will come forth as gold.
Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
11 My feet have followed in His tracks; I have kept His way without turning aside.
Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
12 I have not departed from the command of His lips; I have treasured the words of His mouth more than my daily bread.
Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
13 But He is unchangeable, and who can oppose Him? He does what He desires.
Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
14 For He carries out His decree against me, and He has many such plans.
Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
15 Therefore I am terrified in His presence; when I consider this, I fear Him.
Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
16 God has made my heart faint; the Almighty has terrified me.
Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
17 Yet I am not silenced by the darkness, by the thick darkness that covers my face.
Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.