< Hebrews 10 >

1 For the law is only a shadow of the good things to come, not the realities themselves. It can never, by the same sacrifices offered year after year, make perfect those who draw near to worship.
Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
2 If it could, would not the offerings have ceased? For the worshipers would have been cleansed once for all, and would no longer have felt the guilt of their sins.
Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
3 Instead, those sacrifices are an annual reminder of sins,
Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
4 because it is impossible for the blood of bulls and goats to take away sins.
kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
5 Therefore, when Christ came into the world, He said: “Sacrifice and offering You did not desire, but a body You prepared for Me.
Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
6 In burnt offerings and sin offerings You took no delight.
sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
7 Then I said, ‘Here I am, it is written about Me in the scroll: I have come to do Your will, O God.’”
Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
8 In the passage above He says, “Sacrifices and offerings, burnt offerings and sin offerings You did not desire, nor did You delight in them” (although they are offered according to the law).
Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
9 Then He adds, “Here I am, I have come to do Your will.” He takes away the first to establish the second.
Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
10 And by that will, we have been sanctified through the sacrifice of the body of Jesus Christ once for all.
Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
11 Day after day every priest stands to minister and to offer again and again the same sacrifices, which can never take away sins.
Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
12 But when this Priest had offered for all time one sacrifice for sins, He sat down at the right hand of God.
Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
13 Since that time, He waits for His enemies to be made a footstool for His feet,
Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
14 because by a single offering He has made perfect for all time those who are being sanctified.
kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
15 The Holy Spirit also testifies to us about this. First He says:
Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
16 “This is the covenant I will make with them after those days, declares the Lord. I will put My laws in their hearts and inscribe them on their minds.”
“Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
17 Then He adds: “Their sins and lawless acts I will remember no more.”
Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
18 And where these have been forgiven, an offering for sin is no longer needed.
Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
19 Therefore, brothers, since we have confidence to enter the Most Holy Place by the blood of Jesus,
Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
20 by the new and living way opened for us through the curtain of His body,
kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
21 and since we have a great priest over the house of God,
basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
22 let us draw near with a sincere heart in full assurance of faith, having our hearts sprinkled to cleanse us from a guilty conscience and our bodies washed with pure water.
sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
23 Let us hold resolutely to the hope we profess, for He who promised is faithful.
Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
24 And let us consider how to spur one another on to love and good deeds.
Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
25 Let us not neglect meeting together, as some have made a habit, but let us encourage one another, and all the more as you see the Day approaching.
Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
26 If we deliberately go on sinning after we have received the knowledge of the truth, no further sacrifice for sins remains,
Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
27 but only a fearful expectation of judgment and of raging fire that will consume all adversaries.
Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
28 Anyone who rejected the law of Moses died without mercy on the testimony of two or three witnesses.
Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
29 How much more severely do you think one deserves to be punished who has trampled on the Son of God, profaned the blood of the covenant that sanctified him, and insulted the Spirit of grace?
Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
30 For we know Him who said, “Vengeance is Mine; I will repay,” and again, “The Lord will judge His people.”
Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
31 It is a fearful thing to fall into the hands of the living God.
Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
32 Remember the early days that you were in the light. In those days, you endured a great conflict in the face of suffering.
Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
33 Sometimes you were publicly exposed to ridicule and persecution; at other times you were partners with those who were so treated.
Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
34 You sympathized with those in prison and joyfully accepted the confiscation of your property, knowing that you yourselves had a better and permanent possession.
Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
35 So do not throw away your confidence; it holds a great reward.
Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
36 You need to persevere, so that after you have done the will of God, you will receive what He has promised.
Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
37 For, “In just a little while, He who is coming will come and will not delay.
Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
38 But My righteous one will live by faith; and if he shrinks back, I will take no pleasure in him.”
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
39 But we are not of those who shrink back and are destroyed, but of those who have faith and preserve their souls.
Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.

< Hebrews 10 >