< Genesis 5 >
1 This is the book of the generations of Adam. In the day that God created man, He made him in His own likeness.
Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
2 Male and female He created them, and He blessed them. And in the day they were created, He called them “man.”
Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
3 When Adam was 130 years old, he had a son in his own likeness, after his own image; and he named him Seth.
Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
4 And after he had become the father of Seth, Adam lived 800 years and had other sons and daughters.
Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
5 So Adam lived a total of 930 years, and then he died.
Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
6 When Seth was 105 years old, he became the father of Enosh.
Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 And after he had become the father of Enosh, Seth lived 807 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
8 So Seth lived a total of 912 years, and then he died.
Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
9 When Enosh was 90 years old, he became the father of Kenan.
Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 And after he had become the father of Kenan, Enosh lived 815 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
11 So Enosh lived a total of 905 years, and then he died.
Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
12 When Kenan was 70 years old, he became the father of Mahalalel.
Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 And after he had become the father of Mahalalel, Kenan lived 840 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
14 So Kenan lived a total of 910 years, and then he died.
Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
15 When Mahalalel was 65 years old, he became the father of Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
16 And after he had become the father of Jared, Mahalalel lived 830 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
17 So Mahalalel lived a total of 895 years, and then he died.
Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
18 When Jared was 162 years old, he became the father of Enoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
19 And after he had become the father of Enoch, Jared lived 800 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
20 So Jared lived a total of 962 years, and then he died.
Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
21 When Enoch was 65 years old, he became the father of Methuselah.
Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
22 And after he had become the father of Methuselah, Enoch walked with God 300 years and had other sons and daughters.
Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
23 So Enoch lived a total of 365 years.
Henoko aliishi miaka 365.
24 Enoch walked with God, and then he was no more, because God had taken him away.
Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
25 When Methuselah was 187 years old, he became the father of Lamech.
Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
26 And after he had become the father of Lamech, Methuselah lived 782 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
27 So Methuselah lived a total of 969 years, and then he died.
Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
28 When Lamech was 182 years old, he had a son.
Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 And he named him Noah, saying, “May this one comfort us in the labor and toil of our hands caused by the ground that the LORD has cursed.”
Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
30 And after he had become the father of Noah, Lamech lived 595 years and had other sons and daughters.
Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
31 So Lamech lived a total of 777 years, and then he died.
Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
32 After Noah was 500 years old, he became the father of Shem, Ham, and Japheth.
Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.